Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo
tarehe 23 Machi, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation Bw. Rodger
Voorhies kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani mjini Dodoma.
Makamu
wa Rais amesema amezungumza mambo mengi na Bw. Rodger hasa kwenye
masuala ya afya, uwezeshaji wanawake kiuchumi, kuwatoa kwenye kilimo cha
sasa na kuwaingiza kwenye kilimo biashara lakini pia kuongeza thamani
ya mazao na mambo ya masoko.
Makamu
wa Rais alisema wamezungumza namna ya kuwarasimisha wanawake wa
vijijini na wanawake wakulima ikiwa pamoja na uwezekano wa wanawake
vijijini kuweza kupata mikopo.
Aidha
Makamu wa Rais alizungumzia suala zima la upatikanaji wa maji safi na
salama haswa kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambapo mara kwa mara
kumekuwa na milipuko ya magojwa ya kipindu pindu.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates
Foundation Bw. Rodger Voorhies alisema wamekuja kwa Makamu wa Rais
kuzungumza juu ya shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo hapa nchini
haswa katika masuala ya Kilimo na Afya na Mkakati Mpya wa Kuwawezesha
Wanawake Kiuchumi.
Aidha
wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua kubwa ambayo wamepiga
katika kuwajumuisha wanawake katika masuala yanayohusu Fedha.
Mwisho, Mkurugenzi huyo ameahidi ushirikiano mkubwa kwa Serikali ya Tanzania katika kutekelezaji wa miradi ya taasisi yao.
No comments:
Post a Comment