Katibu
Mkuu Wizara ya Afya ya Malawi Dkt. Charles Mwansambo ametembelea
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ili kupata uzoefu wa namna
Taasisi hiyo inavyotoa huduma za kibobezi (super specialist).
Akizungumza
wakati wa ziara hiyo jana Jijini Dar es Salaam Dkt. Mwansambo alisema
ametembelea MOI ili kuona uwezekano wa kuwaleta wagonjwa wa Malawi
kupata huduma za Kibingwa za Mifupa, Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na
Mishipa ya fahamu badala yakuwapeleka India.
”
Nimefurahi kuona kuwa tuna huduma nzuri za kibingwa kwa jirani zetu wa
Tanzania, hili ni jambo jema na litatupunguzia gharama za kuwapeleka
wagonjwa India badala yake tunawaleta hapa MOI” alisema Dkt.Mwansambo.
Aidha,
Dkt. Mwansambo alipata fursa ya kutembelea vyumba vya upasuaji vya MOI,
vyumba vya wagonjwa walioko katika uangalizi maalum (ICU), wodi za
watoto na wodi maalum za kisasa za kulipia.
Kutokana
na mafanikio ya miundo mbinu ya kisasa yaliyopo MOI Dkt. Mwansambo
ameonyesha dhamira ya dhati ya kuleta madaktari wanafunzi hapa ili
wapate ujuzi wa zaidi.
Naye,
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Mhandisi .Reginald Kimambo alimueleza
Dkt. Mwansambo kwamba huduma zinazotolewa katika hospitali hiyo
zimebobea katika Mifupa, Ajali, Upasuaji wa ubongo, mgongo, mishipa ya
fahamu pamoja na kutua mafunzo kwa madaktari bingwa wa COSESCA.
Ziara
hii imekuja baada ya mkutano wa 65 wa Mawaziri wa Afya wa Ukanda wa
Afrika Mashariki, Kati na Kusini uliofanyika Jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment