KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 18, 2018

TPSF YATAJA SABABU ZA WAFANYABIASHARA KUFUNGA BIASHARA ZAO

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye amesema kinachochangia kufa na kufungwa  kwa biashara nchini kunatokana na  mazingira magumu ya biashara pamoja na sera kandamizi zilizopo.

Amesema utafiti uliofanywa na TPSF umebaini kuwa biashara 4,640 zimefungwa nchini kwa kipindi cha miaka mitatu kutokana na vikwazo mbalimbali, huku akibainisha kuwa mfuko huo kwa sasa upo  tayari kusaidia maeneo mbalimbali ya ujasiliamali pamoja na kutoa elimu.

Simbeye ametoa kauli hiyo jana Mei 17, 2018 katika kongamano la kambi ya ujasiriamali iliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.

Alisema  Tanzania inatakiwa kupiga hatua zaidi katika suala ujasiriamali kwa sababu  ni sekta pekee inayozalisha ajira kwa wingi nchini, hivyo ni vyema ikatumika kitaaluma katika kuwaandaa wanafunzi kufùndishwa kwa vitendo  wanapokuwa vyuoni.

“Sekta binafsi ni mwajiri pekee wa kudumu katika maisha ya mtu ama watu hivyo vijana wetu wanatakiwa kuwa wathubutu na kuondokana na uwoga kwani ni tatizo kubwa kwa vijana wetu,”amlisema Simbeye.

No comments:

Post a Comment