Mbunge
wa Viti Maalumu (Chadema), Sophia Mwakagenda amehoji ni lini Serikali
itazuia ahadi za wagombea urais ambazo zinachukua muda mrefu
kutekelezeka.
Sophia
ameuliza swali hilo bungeni mjini Dodoma leo Alhamisi Juni 7, 2018,
kuwa “Ni lini Serikali itazuia ahadi za wagombea urais ambazo wanatumia
muda mrefu kuzitekeleza kama vile ujenzi wa barabara na zahanati.”
Akijibu
swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, Josephat Kandege amesema
wagombea urais huenda kuuza sera na ilani za vyama vyao ili wachaguliwe
na wananchi.
“Ilani
ni mikataba ya miaka mitano hakuna sababu ya kuzuia kwasababu zimekuwa
zikitekelezwa na mheshimiwa Naibu Spika wewe umekuwa shuhuda wa majibu
yanayotolewa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM,”amesema.
No comments:
Post a Comment