Serikali
kupiti Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi Teknolojia, William Ole Nasha
amesema lengo la serikali huko mbeleni kadiri uwezo utakavyo ruhusu
itatoa elimu bure hadi chuo kikuu.
Nasha
ameyabainisha hayo, leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la
Mbunge George Lubeleje aliyehoji “Kwa kuwa elimu bure ni kuanzia la
kwanza mpaka la 12 lakini kidato cha tano na cha sita hawamo, hawa wote
ni watoto wa mtu mmoja kuna sababu gani za msingi form five na Six
wakaacha kusamehewa karo ? ninaomba Waziri atoe maelezo maana wote
watoto ni wa kwake kwanini hao waachwe?
“Ni
kweli kama alivyosema kwamba watoto wote ni watoto wa Taifa hili
kwahiyo haitakiwi kuwa na ubaguzi, naomba nimuhakikishie Mh. Mbunge ni
kwamba lengo la serikali huko mbele kadiri uwezo utakavyo ruhusu tutatoa
elimu ikiwezekana hadi chuo kikuu bure,” amesema Nasha.
“Lakini
kwasasa kutokana na hali halisi ya kifedha tutaendelea kwanza
kuimarisha miundo mbinu na mazingira katika shule za ngazi ya elimu
msingi kwa maana kwamba kuanzia shule za awali mpaka kidacho cha nne na
kuendelea kutoa elimu bure na uwezo ukiongezeka hatuna shida ya kuongeza
kidato cha tano na cha sita, lakini vilevile kama mnavyofahamu serikali
inatoa mikopo kwaajili ya wanafunzi wa elimu ya juu kwahiyo anachosema
ni kitu cha kweli kwahiyo uwezo ukiongezeka kidato cha tano na sita
elimu bure.”
No comments:
Post a Comment