Baada ya kushuhudia ushiriki mdogo wa
sekta binafsi kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Serikali
imeandaa mpango kabambe wa kuboresha mazingira ya biashara ili kuongeza
ushiriki wao.
Hayo
yamebainishwa leo Juni 14, na Waziri wa Fedha na Mipango, Phillip
Mpango alipokuwa akieleza changamoto zilizojitokeza kwenye utekelezaji
wa miradi ya maendeleo mwaka 2017.
Amesema
mwaka jana serikali imeendelea na ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) ambao
tayari umetekelezwa kwa asilimia 10, kuliimarisha Shirika la Ndege
Tanzania (ATCL) lililonunuliwa ndege moja aina ya Bombardier Q400 na
ujenzi wa kiwanda na shamba la miwa Mkulazi.
"Katika
kipindi hicho kulikuwa na changamoto ya kuchelewa kwa fedha za mikopo
na misaada ya wahisani. Serikali imeandaa mpango kabambe wa kuboresha
mazingira ya ufanyaji biashara nchini ili kuongeza ushiriki wa sekta
binafsi." amesema.
No comments:
Post a Comment