Kamanda
wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi
la Polisi (SACP), Lazaro Mambosasa amewataka watumiaji wa vyombo vya
moto kutompigia simu pindi wakamatwapo na askari wa barabarani kwa kuwa
yeye ndio amewaagiza kufanya kazi hiyo.
Kamanda
Mambosasa ametoa kauli hiyo jana Julai 24, 2018 wakati akizungumza na
waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam na kutaka kila mmoja ambaye
anatumia chombo cha moto kufuata sheria zilizowekwa ili kusudi kuepukana
na ajali zisizokuwa na ulazima ambazo zinapelekea vifo, ulemavu na
utegemezi kwenye familia.
"Ninaomba
nisipigiwe simu juu ya kwamba umekamatwa kwa kosa la usalama barabarani
bali unipigie tu pale unahisi umeonewa. Kwa kuwa wengi wao wanaopigia
simu wametenda makosa ninaomba nisipigiwe kwasababu mimi ndio nawatuma
wawakamate", alisema Kamanda Mambosasa.
Pamoja
na hayo, Kamanda Mambosasa amliendelea kwa kusema; "Jeshi la Polisi
tunaendelea kuhimiza watu kufuata sheria za usalama barabarani, makosa
haya yanafanya watu walalamike kwamba wanakamatwa sana lakini cha ajabu
watu wanaendelea kutenda makosa sana. Bodaboda bado ni tatizo
tunawashuhudia kwenye vivuko 'zebra cross' lakini hata matumizi ya
barabara ya mwendokasi wanavamia na kufanya wanavyotaka".
Kauli
hiyo ya Mambosasa imekuja baada ya kuwepo kwa madereva wa vyombo hivyo
kufanya makosa ya barabarani kwa makusudi kwa kujua yupo mtetezi wao
ambaye ataweza kuwasaidia mara wanapokuwa wamesimamishwa na kukamatwa
barabarani.
Jeshi
la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam kupitia Kikosi chake cha Usalama
barabarani kuanzia Juni 01 hadi Juni 3 mwaka huu wamefanikiwa kukamata
jumla ya magari 42,488 na pikipiki 1,941 kutokana na makosa 73 ya
usalama barabarani na kuingizia mapato Jeshi la Polisi takribani
shilingi Bilioni 2.15 kama tozo zitokanazo na madereva kukiuka sheria za
usalama barabarani.
No comments:
Post a Comment