Rais
wa shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia, ameitaka
klabu ya simba kufanya uchaguzi wao ndani ya siku 75.
Akizungumza
na waandishi wa habari katika makao makuu ya shirikisho hilo, alisema
kwamba kamati ya Uchaguzi ya TFF, wamemfikishia taarifa kwamba Simba
wanatakiwa kufanya uchaguzi wao mkuu.
"Kawaida
huwa ni 60 na ndivyo ninavyojua mimi, lakini Kamati ya Uchaguzi imewapa
siku 75 nazani siku 15 ni za maandalizi, wanatakiwa wafanye uchaguzi
wao mzima ili kupata viongozi wao," alisema.
Mabingwa
wa Ligi Kuu Bara, Simba wapo nchini Uturuki wakiendelea na mazoezi kwa
ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Bara.
Simba
imefikia katika hoteli ya The Green Park Kartepe Resort and Spa iliyopo
katika jiji wa Istanbul Uturuki na watakuwa hapo kwa muda wa siku 16 na
watarudi nchini Agosti 5 siku tatu kabla ya siku ya Simba (Simba Day).
Kocha
msaidizi wa Simba, Mrundi Masoud Djuma alisema hali ya hewa, viwanja na
mahala walipofikia ni sehemu sahihi ya kufanya maandalizi ambayo
wataitumia vizuri kama walivyopanga.
Djuma
alisema mazingira ya hoteli waliyofikia ni nzuri, viwanja vinakizi
kufanya mazoezi magumu na mepesi au programu yoyote ambayo benchi la
ufundi tutakuwa tunahitaji kufanya kulingana na mahitaji yetu ya siku.
No comments:
Post a Comment