KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 5, 2016

SERIKALI YAHAIDI KUBORESHA USIKIVU WA SHIRIKA LA UTANGAZAJI LA TAIFA MIKOA YA PEMBEZONI

SED1
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mhe. Mathew Sedoyeka (kushoto) wakiteta jambo na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye baada ya kuwasili katika Mkoa wa Rukwa jana kuzungumza na wadau wa sekta anazosimamia.

SED2

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na viongozi wa CCM Mkoa wa Rukwa jana wakati wa ziara yake mkoani humo kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia. Kushoto kwa Waziri ni Mwenyekiti wa CCM Rukwa Bw. Hypolitus Matete

SED3

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kushoto) akuzungumza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipofika ofisini kwake wakati wa ziara ya kukutana na wadau wa sekta ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa mawasiliano jana Mkoani Rukwa.

SED4

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizugumza na watendaji kutoka Mkoa wa Rukwa pamoja na wadau wa kada za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo alipokutana nao jana Mkoani hapo kujadili mambo mbalimbali katika sekta hizo pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa mawasiliano.

SED5

Baadhi ya watendaji kutoka Mkoa wa Rukwa pamoja na wadau wa kada za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakimsikiliza kwa makini Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (hayupo pichani) alipofanya ziara yake jana Mkoani Rukwa  kujadili mambo mbalimbali pamoja na kukagua ofisi za TBC na kutoa vitendea kazi kwa Maafisa Mawasiliano wa Mkoa wa Rukwa.

SED6

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiikagua iPad kabla ya kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Zelote Stephen (kushoto) kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi kwa maafisa mawasiliano waliopo Mkoani hapo. Mhe. Nnauye alikabidhi iPad tatu kwa Mkoa wa Rukwa jana baada ya kufanya ziara fupi na kuonana na wadau wa sekta anazozisimamia

SED8

Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Iddi Kimanta akitoa taarifa fupi kuhusu sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  kwa Waziri wa sekta hizo Mhe. Nape Moses Nnauye alipofanya ziara Wilayani hapo jana Mkoani Rukwa.

SED9

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza moja kwa moja kupitia radio ya Wilaya NKasi FM alipofanya ziara katika radio hiyo kuona mafanikio yaliyoletwa na Wilaya ya Nkasi kwa kuwa na radio ya Wilaya.

Picha na: Genofeva Matemu- Maelezo, Rukwa

No comments:

Post a Comment