KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 30, 2016

MBOWE ATANGAZA KUFUTA MAANDAMANO NA MIKUTANO YA UKUTA KESHO, ASEMA WATATUMIA MBINU NYINGINE KUDAI HAKI

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza na Wanahabari leo, Makao Makuu ya chama hicho Jijini Dar Es Salaam.  
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ametangaza kufutwa kwa maandamano na mikutano ya kupinga Udikteta nchini maarufu kama Ukuta na badala yake amesema watatumia mbinu nyingine mpya kuibana serikali.

Amesema walikubalina kuwapa muda viongozi wa dini ili wandeshe majadiliano na serikali yenye lengo la kufikia muafaka lakini hadi sasa anasema hakuna kilichofanyika
“Jana tulikutana tena kupata mrejesho wa swala hilo,taarifa ambayo Kamati Kuu imepewa ni kwamba vingozi wa dini hawakujanya lolote,”.
Ameongeza kusema kuwa wao kama chama cha siasa wanawaheshimu viongozi wa dini na kwamba kwa sasa  wataendelea na harakati  zao za kudai haki kwa kutumia mbinu nyingine.
“Baada ya kuona mambo kadhaa yalitopo tumeamua kusitisha maandamano ya Oktoba Mosi ili  kupisha mbinu nyingine mpya” alisema  
Amefanua kuwa tukio la kudai haki sio tukio la siku moja kama wengi wanavyodhani na kwamba mbinu mpya ni kuyashawishi mataifa ya Ulaya yaibane serikali.
“Chama kilituma Ujumbe maalum Ulaya kuielezea Jamii ya kimataifa ukandamizaji unaoendelea nchini na kwamba misafara mingine ya chama itaendelea kwenda nchi nyingi zaidi kufanya mikutano na Jumuiya ya kimataifa na kuifahamisha kwamba Tanzania ile ya amani haipo tena,” alisema
Pia alisema wanaendelea na maandalizi ya kufungua kesi mbalimbali kuhusu yanayoendelea nchini.CHANZO HABARI24
          


No comments:

Post a Comment