KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 30, 2016

WATATU WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI ARUSHA KWA K0SA LA KUGHUSHI

kamanda-charles-mkumboNa Mahmoud Ahmad,Arusha
Jeshi la polisi mkoani Arusha linawashikilia watu watatu kwa kosa la kughushi nyaraka za ofisi na kupelekea wizi wa jumla ya kiasi cha sh,50 milioni mali ya chama cha wakulima cha Tanganyika(TFA).
 
Kushikiliwa kwa watuhumiwa hao kunakuja zikiwa ni siku chache tu baada ya jeshi hilo  kumshikilia na kisha kumwachia kwa dhamana aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya muda wa TFA ,Meynard Swai kwa tuhuma za ubadhirifu wa mali na fedha ndani ya chama hicho.
 
Mwenyekiti huyo alishikiliwa kwa siku kadhaa na jeshi la polisi mkoani hapa mwezi uliopita jijini na kisha kuhojiwa kabla ya kuachiwa kwa dhamana ambapo kwa sasa polisi bado wanaendelea na uchunguzi dhidi ya mashtaka yanayomkabili.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,Charles Mkumbo alisema kwamba watuhumiwa hao walishikiliwa katika maeneo tofauti hapa nchini.
 
Aliwataja kwa majina walioshikiliwa kuwa ni Salvatory Mwandu,Simon Mwandu pamoja na mkazi wa jijini Dar es salaam,Jesca Canisius ambao kwa sasa wameachiwa kwa dhamana.
 
Mkumbo,alisema kwamba watuhumiwa hao wako chini ya uchunguzi na jeshi lake na bado linaendelea na upelelezi wa kina huku akisisitiza ya kwamba hawatasita kumchukulia hatua za kisheria mtu yoyote atakayevunja sheria za nchi.
 
“Jeshi la polisi linaendelea na upelelezi wa tuhuma hizo na linatoa

No comments:

Post a Comment