KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 19, 2017

MGODI WA BUZWAGI MBIONI KUFUNGWA

SASU
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini, Doto Mashaka Biteko (wa pili kushoto) akimsikiliza Meneja wa Mgodi wa Buzwagi, Assa Mwaipopo (hayupo pichani) akielezea shughuli za uzalishaji wa Dhahabu katika Mgodi huo. Kushoto kwake ni Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje na wengine ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Nishati na Madini, Watumishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Wafanyakazi wa Mgodi wa Buzwagi.
SASU 1
Kaimu Kamishna wa Nishati na Madini, Ally Samaje (anayetoa maelezo) akielezea Mpango wa Serekali wakati wa kufunga Mgodi wa Buzwagi. Wengine katika picha ni Wabunge kutoka Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini, Watumishi wa Wizara ya Nishati na Madini na Viongozi Waandamizi kutoka Mgodi wa Buzwagi.
SASU 2
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Ntalikwa (katikati) akiwa anafanya majadiliano na Kaimu Kamishna wa Madini, Ally Samaje na Mbuge wa Kahama Jumanne Kishimba Mara baada ya kutembelea mgodi wa Buzwagi.
SASU 3
Wataalamu kutoka Idara ya Madini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutoka katika eneo la uzalishaji wa Dhahabu.
SASU 4
Muonekano wa Mgodi wa Buzwagi katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga,
SASU 5
Kotena iliyofanyiwa maandalizi tayari kupokea makinikia ya Shaba ambayo yanachimbwa kwa asilimia kubwa katika Mgodi wa Buzwagi.
SASU 6
Kotena ambayo tayari imejazwa na makinikia ya Shaba tayari kwa ajili ya kufunga ili kusafirishwa nje.
SASU 7
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Ntalikwa (wa pili kushoto) akimsikiliza Kaimu Kamishna wa Madini Mhandisi Ally Samaje, kabla ya kusikiliza mada kutoka kwa Meneja wa Buzwagi.
SASU 8
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini, Doto Mashaka Biteko (wa pili kulia) akiwa na wanakamati wezake wakiongozana na Viongozi Waandamizi kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Mgodi wa Buzwagi mara tu baada ya kuwasili katika Mgodi huo. 
……………………

No comments:

Post a Comment