Mwanamuziki
anaefanya vizuri katika nyimbo za injili, Godlucky Gosbeth amefunguka
na kusema kuwa hakuamini alipokuatana na raisi katika sherehe za
uzinduzi wa taasisi ya Jakaya Kikwete iliyofanyika juzi jijini Dar
es salaam.
Godlucky
anasea kuwa kwake ni bahati sana na hakutegemea kama angeitwa pale
mbele kwa ajili ya kusalimiana na viongozi wakubwa wa serikalai mpaka
alipotoka ikulu ndipo alipoaanza kuamini kuwa ni kweli jambo lile
limetendeka.
Godluck
anasema kuwa , kuonekana kwake na kusalimiana na viongozi wakubwa
imemfanya apokee simu nyingi sana zikimpongeza kwa kazi hiyo nzuri
aliyoifanya na hata yeye pia anashukuru Mungu kwa kuwa anazidi
kumbariki.Godlucky aliyaongea hayo alipokuwa akiongea na radio clouds
fm.
Hata
katika ukurasa wake wa instagram , Gudluck aliandika maneno ya
kumshukuru Mungu kwa kuandika kuwa katika maisha yake hakuwahi kuwaza
kama kuna mambo makubwa kama hayo yangeweza kutokea katika maisha yake
lakini anachoamini ni kwamba Mungu amekuwa akitimiza ahadi alizokuwa
ameweka kumtimizia maishani mwake.
No comments:
Post a Comment