KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 19, 2014

SERIKALI YASISITIZA MISHAHARA YA WATUMISHI KULIPIWA BENKI


 


Serikali imeagiza watumishi wote wa umma walipwe mishahara moja kwa moja kupitia akaunti zao sahihi za benki ambazo zitatumika kupitishia mihahara yao.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Fedha Mwigulu Nchemba (Pichani) alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisi za Hazina leo jana Dar es salaam.

“Mishahara ya Watumishi wote wa Serikali, Wakala na Taasisi za umma italipwa moja kwa moja kupitia akaunti zao za benki” alisema Mwigulu.

Ili kufanikisha azma hiyo ya Serikali, Mwigulu aliwaagiza waajiri wote wa sekta ya umma kuwa wawe na akaunti namba za benki za watumishi wao wote walio chini ya fungu husika ambazo zina taarifa sahihi na wakizingatia mfumo sahihi wa taarifa za kiutumishi.

Mwigulu alionya kuwa mtumishi asiye na akaunti benki asilipwe mshahara wake dirishani ambapo amewahimiza waajiri kuwasisitiza watumishi walio chini yao kufungua akaunti sahihi ya benki kwenye mfumo ambayo itatumika kulipa mshahara husika kupitia orodha ya malipo ya mshahara (payroll) inayotolewa na Hazina.

Aidha, Mwigulu amasema kuwa kila ifikapo tarehe 10 ya kila mwezi  waajiri wote wawe wamewasilisha maombi ya fedha za kulipa mishahara kwa mwezi unaohusika wakiambatisha orodha ya malipo ya  watumishi ya kuthibitisha kiasi kinachoombwa.

“Waajiri watakaoshindwa kutoa ‘Payroll’ watasababisha watumishi wanaowaongoza kushindwa kupata mishahara yao kwa mwezi husika jambo ambalo sio nia ya Serikali” alisisitiza Mwigulu.

Utaratibu huu wa kulipa mishahara utakuwa endelevu na umedhihirisha kuwa na tija kwa matumizi ya fedha za umma kwani umeonesha mafanikio ambayo kwa mwezi wa saba na wa nane hakuna mtumishi, Wakala za Serikali wala Taasisi iliyolalamika kukosa mishahara.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment