Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Sigh Seth (kushoto), akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 20, kwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto (wapili kulia), ikiwa ni mchango wa IPTL kusaidia maandalizi ya Tuzo za wanamichezo bora nchini. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Makamu Mweyekiti wa TASWA, Egbert Mkoko, Katibu Mkuu, Amir Mhando na Mwanasheria na Mshauri Mkuu wa IPTL, Joseph Makandege, na kulia ni Mjumbe wa TASWA, Rehure Richard Nyaulawa
Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto, akizungumza na Wanahabari baada ya kupokea fedha hizo.
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Sigh Seth, akiwaeleza Wanahabari
furaha yake ya kuisaidia TASWA kitita hicho cha fedha, kusaidia
wanamichezo ambapo nae alikiri kuwa yeye ni miongoni mwa wanamichezo na
amewahi kuwa Mshindi wa tatu wa Mbio za Magari Afrika.
Waandishi wa Habari wakiingia kuangalia uzalishaji wa umeme katika mitambo ya IPTL.
No comments:
Post a Comment