Mkurugenzi wa kampuni ya Mobile Solution,Dimitrios Lintis(katikati)akiwaonyesha namba ya mshindi wa Promosheni ya JayMillions Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha Tanzania Mrisho Millao na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(Kulia) wakati wa kuchezesha droo ya 13 iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo Mkazi wa Magu James Mangu amejishindia kitita cha shilingi Milioni 10/- Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544. |
Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha Tanzania Mrisho Millao(Kushoto)akihakiki namba ya simu ya mshindi wa promosheni ya JayMillions anayoonyeshwa na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(Katikati)wakati wa kuchezesha droo ya 13 iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo Mkazi wa Magu James Mangu amejishindia kitita cha shilingi Milioni 10/-anaeshuhudia kulia ni Afisa wa kampuni hiyo Pristin Lyatonga.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544. |
Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom
Tanzania,Matina Nkurlu (Katikati) akiongea na mshindi wa kitita cha
shilingi Milioni 10 kupitia promosheni ya JayMillions Mkazi wa Magu
mkoani Mwanza James Mangu.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa
kutuma neno Jay kwenda 15544. Mkazi
wa Wilaya ya Magu mkoani Mwanza James Mangu,
leo ameibuka mshindi wa shilingi milioni 10 katika droo ya kumi tatu
ya promosheni ya Jaymilioni inayoendeshwa na kampuni ya mawasiliano ya
Vodacom Tanzania.
Mangu
ambaye ni baba mwenye watoto 4 ambaye pia ni mjasirimali amesema kuwa
amepokea taarifa hizi kwa furaha akiwa katika kazi zake za biashara
na amefurahia ushindi huu ambao anaamini utabadilisha maisha yake kwa
kiasi kikubwa.
“Kwa
muda mrefu nimekuwa nikihangaika na biashara na kukumbana na changamoto
nyingi kama vile ukosefu wa mtaji.Kwa ushindi huu naamini nitaboresha
shughuli zangu za biashara ikiwemo kuanzisha biashara ya kuuza dawa za
binadamu biashara ambayo nilikuwa naota kuifanya kwa muda
mrefu”.Alisema Mangu kwa furaha.
Mbali
na kuanzisha biashara amesema fedha zake zitamsaidia kulipia watoto
wake ada za shule ikiwemo kuboresha makazi yake “.Nashukuru Vodacom kwa
kuleta promosheni hii ambayo naamini itabadilisha maisha yangu.
Aliongeza
kuwa kwa muda mrefu amekuwa akishiriki kwenye promosheni mbalimbali na
hajawahi kufanikiwa kwa ushindi huu anaamini kuwa promosheni hizi
hususani za Vodacom ni za kweli na amewataka wateja wote kushiriki ili
kutopoteza bahati zao za kujishindia mamilioni ya fedha na kubadilisha
maisha yao.
Akiongea
muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi,Meneja Uhusiano na Mawasiliano
ya Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu amempongeza mshindi na
kuwahimiza wateja wote wa Vodacom kuchangamkia promosheni hii kwa
kuhakikisha wametuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza nafasi
zao za kushinda pia alisema kuwa njia nyingine ya kushinda ni kutuma
neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha
ambapo mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-
Alisema
kuwa tangu promosheni hii ianze mapema mwezi huu tayari mteja 1 mkazi
wa mkoa Katavi,Hynes Kanumba,amekwishajishindia milioni 1 na wateja
watano wameishajishindia shilingi milioni moja kila mmoja na maelfu
wengine tayari wamejishindia muda wa maongezi.
“Promosheni
hii itadumu kwa muda wa siku mia moja hivyo leo ni droo ya kumi na tatu
hivyo bado kuna mamilioni ya fedha yamewasubiri watanzania,wanachopaswa
kufanya ni kuhakikisha
kila siku wameangalia kama namba zao zimeibuka na ushindi kwenye droo
ya siku kwa kutuma neno Jay kwenda namba 15544. Promosheni hii inayoendelea ya
Jaymillions inawahusisha wateja wote wa Vodacom ,kiasi kikubwa
cha fedha kitaendelea kutolewa kila siku na ni rahisi kabisa kila mtu
kushiriki. Mara tu ujumbe huu unapotumwa, mteja atapokea ujumbe mfupi
utakaomjulisha kama ameshinda na ikiwa hajashinda
siku hiyo atajulishwa hivyo na kuambiwa ajaribu tena siku inayofuata.
Kila SMS itagharimu Sh. 300/- tu”.Alisema.
Vodacom
imepanga kutoa mshindi mmoja wa Sh. 100m/-, washindi kumi wa Sh. 10m/-
na washindi thelathini wa Sh. 1m/- KILA SIKU kwa siku mia moja! Pia
washindi elfu
kumi watapokea muda wa maongezi wa bure wenye thamani ya Sh. 1000/-
|
No comments:
Post a Comment