![]() |
| Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta akizungumza wakati wa ziara ya kikazi Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Dar es Salaam jana, baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi. Kalia ni Mkurugenzi Mkuu wa (TPA) Mhandisi Madeni Kipande. Picha na Venance Nestory |
Waziri Sitta alisema hayo jana wakati akizungumza
na watendaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), katika
mfululizo wa ziara zake kwa mashirika, taasisi na mamlaka zilizo chini
ya wizara yake kwa lengo la kufahamiana na kujua changamoto na kupanga
mikakati yake katika utendaji.
Akizungumza katika mkutano na watendaji TPA, baada
ya kusikiliza taarifa ya utendaji kazi iliyohusisha mikakati, mafanikio
na changamoto za mamlaka hiyo, Sitta alisema duniani kote bandari ni
kitovu cha uchumi wa nchi.
Alisema vitendo vyovyote vya udokozi na hujuma
vinavyofanywa na watumishi wasio waaminifu ni kuhujumu uchumi wa Taifa,
hivyo angependa kuona wahusika wanashtakiwa na kunyimwa dhamana.MWANANCHI



No comments:
Post a Comment