KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 31, 2015

TEKNOLOJIA! BIBI KIZEE AANGUKA AKIWA ANASAFIRI ANGANI


  

SAM_2318
Na Kadama Malunde, Shinyanga KATIKA hali ya kushangaza, bibi kizee anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka (70), asiyejulikana jina wala makazi yake, ameanguka akiwa uchi wa mnyama nyumbani kwa Suzana Mwandu, mkazi wa Mtaa wa Mageuzi mkoani Shinyanga.
Tukio hilo lilitokea juzi ambapo bibi huyo baada ya kuanguka alianza kutembelea makalio bila kuzungumza chochote jambo ambalo limedaiwa ni ushirikina.
Akielezea tukio hilo jana, Mwandu alisema lilitokea nje ya nyumba ambapo alishangazwa kumkuta kikongwe huyo akiwa amelala huku akiwa uchi wa mnyama.
Mwandu alisema baada ya kikongwe huyo kuanguka, alijivuta hadi kwenye jiko lake lililoko nje ya nyumba ambalo lipo wazina baada ya kuanza kumsemesha ndipo akazinduka na kuanza kuongea maneno yasiyoeleweka, hali ambayo ilimtia wasiwasi na kutoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya Mtaa.
“Nyumba yangu nimeizindika vilivyo, hivyo kikongwe huyu alipokuwa katika safari zake na kupita maeneo ya nyumbani kwangu ndipo akakutana na balaa hilo na hatimaye akajikuta ameanguka na kuingia jikoni kwa ajili ya kujificha.

“Unajua siku zote mchawi anapoanguka na ukimwacha kwa muda mrefu bila ya kumsemesha, anaweza kupoteza maisha, hivyo kutokana na mimi kutokuwa na ubaya naye, nikaona bora nimsemeshe ili kumwokoa na baada ya hapo nikampa nguo za kujistiri na aibu ya kuwa mtupu,” alisema Mwandu.
Kwa upande wao mashuhuda wa tukio hilo, walidai kuwa bibi huyo huenda akawa ni mchawi kutokana na kauli zake tatanishi alizokuwa akizitoa huku mikono yake ikionekana kukatwa kwa mapanga na kuota sugu.MTANZANIA

No comments:

Post a Comment