KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 23, 2015

YULE MWENYEKITI WA SERIKALI YA MTAA MIGOMBANI ALIYEAPISHWA NA WANANCHI BAADA YA KUCHOSHWA NA MIZENGWE, SASA AMEAPISHWA RASMI NA HALMASHAURI YA ILALA


Pg 1
 Hapa akiapishwa na wananchi
 Wakati Mwenyekiti wa Mtaa wa Migombani-Segerea, Dar es Salaam, Japhet Kembo, aliyejiapisha kwa kutumia wakili binafsi akiapishwa tena jana na wakili aliyechaguliwa na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi ameonya vitendo vya wadau wa siasa kujichulia sheria mikononi na kuwataka wafuate sheria na taratibu.
Kembo aliyejiapisha mwanzoni mwa wiki hii, alijumuika na wenzake kutoka mitaa ya Migombani - Kiwalani na Kigogo Fresh B katika tukio lililoshuhudia mwenyekiti mteule wa Kigogo akishambuliwa na wafuasi wa Ukawa na kuzuia uapishwaji wake. Baada ya kuapishwa, Kembo alisema sasa yupo rasmi kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wake waliomchagua kwani siku zote alikuwa na shauku ya kuingia ofisini kuanza kazi.
Wakati hilo likikamilika, wafuasi wa Ukawa walimshambulia na kuzuia kuapishwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Kigogo Fresh B, Mariano Maurus wa CCM kwa madai kuwa hakushinda nafasi hiyo.
Mwenyekiti huyo aliachwa kiporo kutokana na utata wa matokeo kwenye uapishaji wa wajumbe wa Manispaa ya Ilala. Wakati akishambuliwa na kuondolewa eneo la tukio, aliwaacha wenyeviti wenzake wawili; Kembo na Ubaya Chuma wa Migombani - Kiwalani wakikamilisha mchakato huo pamoja na wajumbe 15 wa mitaa yote mitatu.
Mwanasheria wa manispaa hiyo, Mashauri Musimu alisema pamoja na yote yaliyotokea kwa mwenyekiti huyo, Maurus ndiye anayetambulika kutokana na kumbukumbu za matokeo zilizopo hivyo lazima ataapishwa ili awatumikie wananchi.
Shambulizi hilo lilitokea jana asubuhi wakati wajumbe wakiitwa kuingia ukumbini na lilipoitwa jina Maurus alishambuliwa na baadhi ya makada waliokuwapo eneo hilo kabla askari hawajamwokoa, akiwa ameshachaniwa nguo.
Jaji Mutungi
Akizungumzia tukio la kujiapisha, Jaji Mutungi alisema ingawa kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mtaa zinampa mamlaka wakili, hakimu wa Mahakama ya Mwanzo na ya wilaya kuwaapisha viongozi waliochaguliwa, kuna utaratibu ambao lazima ufuatwe.

No comments:

Post a Comment