Kada wa CCM Mzee Kingunge Ngombale Mwiru akisalimiana na Waziri wa
Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa wakati shughuli za
kutoa heshima za mwisho msiba wa Captain John Komba katika viwanja vya
Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Rais mtsaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamin William Mkapa akisalimiana na Mzee Kingunge alipowasili kwenye viwanja hivyo.
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mtungi (kulia)
akiteta jambo na Mwenyekiti Mtendaji wa makapuni ya IPP, Dkt. Reginald
Mengi (katikati) pamoja na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dkt.Shukuru Kawambwa.
Naibu wa Waziri wa Fedha ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM), Mh. Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Katibu Mkuu wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbrod Slaa.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida (kushoto)
akiteta jambo na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha
Mapinduzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Dodoma na
Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Mh.Adam Kimbisa, akifuatiwa na
Mbunge wa Jimbo la Simanjiro Ndugu Christopher Ole Sendeka, kabla ya
kuanza ibada maalum ya kuaga mwili wa marehemu Capt. John Komba. katika
viwanja vya Karimjee jijini Dar leo.
No comments:
Post a Comment