KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 13, 2015

ABIRIA 18 WAUAWA AJALI YA BASI,FUSO


Basi la Nganga linalofanya kazi zake kati ya Mbeya na Morogoro likiwa linawaka moto mara baada ya kugongana na lori. Picha na mtandao 

Morogoro. Watu 18 wameteketea kwa moto baada ya basi la Kampuni ya Nganga Express na lori aina ya Fuso kugongana uso kwa uso na kuwaka moto katika eneo la Iyovi, Milima ya Uduzungwa, Morogoro
Katika ajali hiyo iliyotokea jana saa mbili asubuhi, abiria 15 waliokuwa kwenye basi na wengine watatu wa lori waliteketea kwa moto huku wengine 10 wakijeruhiwa vibaya.
Taarifa na picha za ajali hiyo zilianza kusambaa jana asubuhi kupitia mitandao ya kijamii zikionyesha masalia ya miili ya walioteketea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonard Paul alisema ajali hiyo ilitokea baada basi hilo lililokuwa linatoka Kilombero kwenda Mbeya likiwa kwenye mistari ya barabarani ya katazo na kwenye mwendo kasi kugongana na lori lililokuwa limebeba matikiti na kuwaka moto.
Alisema majeruhi wanne wamelazwa katika Hospitali ya St. Kizito, Mikumi na sita wako katika Hospitali ya Mtandika, Iringa.
Alisema kwenye basi hilo kulikuwa na pikipiki ambayo pia iliungua na kusema inawezekana ndiyo iliyosababisha moto huo.
Ajali hiyo ni mfululizo wa ajali zinazotokea katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwa ni siku moja baada ya watu watano kufariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mikoa ya Dodoma na Iringa saa 36, baada ya kumalizika mgomo wa madereva nchini.MWANANCHI

No comments:

Post a Comment