KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 9, 2015

JOTO LA UBUNGE SIMANJIRO LAZIDI KUSHIKA KASI

unnamed
Mahmoud Ahmad,Arusha
Joto la ubunge katika jimbo la Simanjiro mkoani Manyara limezidi kushika kasi mara baada ya mkuu wa wilaya ya Kakonko,Peter Toima   kutamka ya kwamba endapo wakazi wa jimbo hilo watamshawishi na yeye kushawishika basi atafanya  uamuzi mgumu wa kuchukua fomu kwa niaba yao muda ukiwadia.
 
Toima,alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati alipozungumza na Fullshangwe katika jiji la Arusha ambapo alisistiza kuwa amekuwa akipokea maombi mengi kutoka kwa makundi mbalimbali wilayani humo ya kumtaka achukue fomu ya ubunge mwaka huu.
 
“Kama watu wa Simanjiro wakifanikiwa kunishawishi na nikashawishika ,nitatii sauti yao na nitafanya uamuzi kwa niaba yao muda ukiwadia’alisema Toima
 
Alisema kuwa mara kwa mara amekuwa akijiuliza ni kwanini wakazi wa wilaya hiyo wamekuwa wakimtaka achukue fomu ya kuwania ubunge wa jimbo hilo na kusema amebaini chanzo kinatokana na wao kuchoshwa na uongozi uliopo kwa kuwa hakuna mabadiliko.
 
Alisema kuwa anasubiri muda ukifika atafanya maamuzi magumu kwa kuwa kitendo cha wakazi hao kumpelekea maoombi hayo ni mapenzi yao na msukumo wao ili kukidhi mahitaji yao.
 
“Watu wa Simanjiro wanatamani kwamba ningekuwa mbunge wao mimi nasema hayo ni mapenzi yao,msukumo wao ili kukidhi mahitaji yao”alissiitiza Toima

No comments:

Post a Comment