KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 9, 2015

KUTOKA UTT-AMIS: KUMBE UNAWEZA UKAWEKEZA FEDHA ZAKO UTT-AMIS NA UKAISHI KAMA BABA MWENYE NYUMBA JIJINI!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjDz7LhpWWiGgPGf1VOtETLGHIfL7nK8_6_ky5zSYQ_0aHT-p7_QLKZFGxNjBFZRsxsSJx0N0O7EHU9WTd7tA1DlgL2FwN_QSC5Cq3YnarBRpGcFrSoXXwoJB0famG58p4g9HeXJjsDkZw/s1600/IMG-20141025-WA0006-1.jpg
Mkurugenzi wa Masoko na Uhusiano UTT-AMIS, Daud Mbaga (aliyesimama kushoto), akitoa elimu ya uwekezaji wa pamoja kwa wakazi wa Mbeya waliotembelea maonyesho ya kitaifa ya Biashara kwenye ukumbi wa Mkapa, Soko la Matola.                             



Swali :Una wito kwa jamii? (Mbaga anajibu)

Jibu: Wito wangu kwa jamii ni wachangamkie uwekezaji huu kwani unatoa faida nzuri, na usalama wa uwekezaji umezingatiwa, na isitoshe swala zima la ukwasi limepewa uzito mkubwa. Tuchukue mfano wa kujenga nyumba, kila mtu anapenda awe na nyumba nyingi na bora. Leo hii viwanja katikakati ya jiji ni bei sana hivyo ukiwa na shilingi milioni mia moja utajenga nyumba hiyo nje kidogo ya mji na utaipangisha na kupata fedha kati ya laki tano hadi sita kwa mwezi .Lakini je ni rahisi kupata fedha hii ya mkupuo?Aghalabu kwa watakaoweza ni wachache.

Hivyo watumie mifuko hii kuweza fedha zao na kukuza mitaji ili waweze kufanya uwekezaji kama huo wa kujenga nyumba. Lakini pia mwingine anaweza wekeza kiasi hicho kwa mkupuo cha shilingi milioni mia  moja kwenye  mifuko na kikampatia faida sawa au zaidi ya shilingi laki sita kwa mwezi,  ambapo ni sawa na bei ya kupangisha nyumba aliyojenga kwa kiasi cha shilingi milioni mia moja hizohizo.  Kumbe basi wakati mwingine kupitia mifuko ya UTT -AMIS unaweza pata faida shindani na kukurahisishia njia mbadala za kupata kipato.  Mfano Mfuko wa Umoja umekuwa ukikua kwa zaidi ya wastani wa asilimia 30 kwa kila mwaka tokea uanzishwe mwaka 2005



No comments:

Post a Comment