![]() |
| Timu ya Yanga imeweza kuvuka hatua ya 16 bora michuano ya kombe la
shirikisho baada ya kufungwa goli 1-0 na timu ya Platnum ya Zimbabwe
katika mechi ya marudiano iliyochezewa katika uwanja wa Zvishavane
nchini Zimbabwe. Mechi ya kwanza ya timu hizo iliyochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, timu ya Yanga ilishinda bao 5-1 dhidi ya timu hiyo ya Zimbabwe na kufanya timu ya Yanga kuibuka mshindi wa jumla ya mabao 5-2 dhidi ya Platnum, Mchezaji Walter Msoma wa Platnum ndiye aliyeifungia timu hiyo bao kunako dakika ya 29 akipokea pasi kutoka kwa Donald Ngoma. Kipa wa Yanga Ally Mustafa Mtinge "Barthez" ndiye aliyekua nyota wa mchezo kwa kuokoa mipira mingi ya hatari likiwemo shuti la Donald Ngoma alilopiga ndani ya 18 na kipa huyo wa wanajangwani kuokoa kwa mguu. |
April 4, 2015
YANGA SONGA MBELE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment