KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 18, 2015

JAJI MKUU MSTAAFU AJITOSA URAIS CCM.

Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani.                                                                                   "Nilirudia uanachama wangu wa CCM mwaka 2011, baada ya kustaafu wadhifa niliokuwa nao kama Jaji Mkuu... Sina doa katika serikali au utumishi wangu; kwa kweli hakuna Mtanzania anayeweza kuninyooshea kidole kwa kupokea au kuhusika na vitendo vya rushwa. Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza..."
 
Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhan, ametangaza nia ya kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku akieleza kuwa licha ya kuwapo kwa utitiri wa wagombea urais, hakuna Mtanzania yeyote anayeweza kumnyooshea kidole akimtuhumu kupokea au kuhusika na vitendo vya rushwa.
 
Jaji Ramadhan ambaye ni kada wa 36 kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama chake kuwania kiti hicho, alisema hakuna mgombea anayemtisha kati ya wote waliomtangulia, kwa kuwa hakuna mwanajeshi anayeogopa.
 
Jaji Ramadhani alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana katika Makao Makuu ya CCM Mjini Dodoma, muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo.
 
“Sina doa katika serikali au utumishi wangu; kwa kweli hakuna Mtanzania anayeweza kuninyooshea kidole kwa kupokea au kuhusika na vitendo vya rushwa. Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza. Mimi ni mwanajeshi, nimestaafu nikiwa Brigedia Jenerali Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Sijui kama kuna mwanajeshi anayeogopa na hakuna mgombea ninayemuogopa; nikiogopa ina maana mimi si mwanajeshi,” alisema na kuongeza: 
 
“Nina uzoefu wa kutosha, nina uwezo wa kuwatumikia Watanzania twende huko tunakotaka na kuinua uchumi wetu. 
 
Nimejipima na nimeona nina uwezo wa kugombea urais kwa sababu nakidhi vigezo vyote vinavyotakiwa kisiasa na kiuongozi; kilichonisukuma kutangaza nia ya kugombea ni uwezo wangu, sijashinikizwa na mtu yeyote,” alisema Jaji Ramadhani.
 
KUJIUNGA NA CCM
Kuhusu utata alijiunga lini na CCCM, wakati amekuwa mtumishi wa umma kwa zaidi ya miaka 33, Jaji Ramadhani alisema:
“Nilijiunga na CCM mwaka 1969 nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa tatu Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na niliendelea na uanachama wangu hadi 1992 kipindi mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa na kusababisha mabadiliko ya Katiba ambayo yaliweka masharti kwa mtumishi wa umma kutokuwa mwanachama.”
 
Jaji Ramadhani alisema baada ya mabadiliko hayo, uanachama wake ndani ya CCM ulisimama hadi mwaka 2010 alipostaafu nafasi ya Jaji Mkuu wa Tanzania na kulazimika kurejesha uanachama wake mwaka 2011 kwa ajili ya kuendelea na masuala ya siasa.
“Nilirudia uanachama wangu wa CCM mwaka 2011, baada ya kustaafu wadhifa niliokuwa nao kama Jaji Mkuu”.
 
RUSHWA
Kuhusu rushwa, alisema ni tatizo kubwa nchini. “Tatizo la rushwa katika serikali na nchi yetu ni kubwa, nataka nilimalize kama chama changu kitaniteua na kushinda nafasi hiyo…wakati nilipokuwa Jaji Mkuu, nilipambana nalo katika mahakama zetu,” alisema na kuongeza:
 
"Nawahakikishia Watanzania nikiwa Rais, ukila rushwa Kilimanjaro, hutahamishiwa Mtwara maana hata waliopo Mtwara ni Watanzania, hawataki mla rushwa.”
 
KATIBA MPYA
Alipoulizwa msimamo wake kuhusu mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya, Jaji Ramadhani alisema: “Kwa nafasi yangu niliyokuwa nayo kama Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, kazi yetu ilikwishamalizika, baada ya kumkabidhi Rais Jakaya Kikwete, Rasimu ya Pili ya Katiba pale kwenye ukumbi wa Karimjee na Bunge Maalum la Katiba limemaliza kazi yake, hatua iliyobaki ni wananchi kuamua katika Kura ya Maoni. Na ndiyo itakayoamua hatma ya Katiba Mpya na si Rais.”

No comments:

Post a Comment