![]() |
| Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, amewataka wana-CCM kuikosoa serikali pale inapokosea badala ya kuisifu hata kwa mabaya.
Amesema kitendo cha kuisifia serikali hata inapokosea husababisha kukosekana kwa utendaji kwa viongozi walioko madarakani.
"Serikali inakosea na ni wajibu wa CCM kuikosoa badala ya kusubiri
wapinzani waandamane na kufanya hivyo ni kuongeza utendaji wa viongozi
na watendaji walioko serikalini," alisema.
Kinana aliyasema hayo juzi wakati akihutubia wananchi wa Wilaya ya
Chato kwenye viwanja vya kituo cha mabasi cha zamani baada ya kuanza
ziara ya siku saba mkoani Geita akitokea mkoani Kagera.
Alisema hakuna sababu wala faida ya kuisifu serikali ambayo kila
mara inaboronga hali ambayo inasababisha wananchi kukichukia chama hicho
kwa sababu ndicho chenye serikali.
"Lazima wana-CCM tujifunze kuikosoa serikali, haiwezekani kila mara
tuwe na kazi ya kuisifia tu hata kama ikikosea, serikali ni ya chama
chetu, hatuwezi kusifia maovu na pale serikali itakapofanya vizuri
tutaisifia," alisema Kinana.
Alisema hakuna serikali inayoomba kura isipokuwa chama ndicho
kinaingia dhamana na wananchi wakati wa kuomba ridhaa ya kuwatumikia.
"Wakati tunaomba kura, hawa watendaji wa serikali wanakuwa
wametulia hawana habari, sisi ndiyo tunatumia nguvu kubwa kuomba ridhaa,
tunapochaguliwa ndiyo tunachagua watendaji wa kufanya nao kazi
tunapounda serikali, hivyo ni wajibu wetu kuikosoa," alisema Kinana.
Kwa upande wake, Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape
Nnauye, alisema mwaka 2012 waliweka maazimio ya kukitoa chama ofisini na
kukipeleka kwa wananchi, hali ambayo imekifanya kiimarike.
Alisema chini ya Katibu Mkuu wake Kinana, wamefanya mambo makubwa
ikiwamo kuwafikia wananchi na kukifufua Chama kwani kilishapoteza
mwelekeo pamoja na kuikosoa serikali.
|
June 17, 2015
KINANA: WANA - CCM IKOSOENI SERIKALI IKIKOSEA SIYO KUSIFIA TU.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment