KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 19, 2015

MUUAJI WA WATU TISA KANISANI AKAMATWA

Baby-faced 'killer': Dylann Storm Roof held court papers in his cuffed hands as a police officer held him by a chain
Mshukiwa wa mauaji Storm Roof (21) akiwa ameshikilia karatasi za mahakama.
Prison stripes: Roof, 21, is pictured being escorted onto a plane to be extradited to South Carolina on Thursday
Storm Roof akiwa amesindikizwa na polisi kwenye ndege kwa safari ya kurudishwa Carolina Kusini. 
All smiles: Roof appeared to smile as he was hauled away from the Shelby Police Department in North Carolina at noon on Thursday
Muuaji wa Watu tisa alionekana anatabasamu baada ya kukamatwa na polisi.   


Mshukiwa wa mauaji ya watu tisa katika kanisa moja la kihistoria mjini Carolina Kusini amekamatwa.

Kulingana na mwanasheria mkuu Lorreta Lynch, awali maafisa walimtaja kijana huyo wa miaka 21 kuwa Dylann Storm kama mtu waliyekuwa wakimsaka kwa shambulizi la Charleston. 

Maafisa wa polisi wanasema kuwa mshukiwa huyo aliyejihami na bunduki aliketi katika mkutano wa mafundisho ya biblia kwa takriban saa moja kabla ya kufyatua risasi na kuwaua wanawake sita na wanaume watatu akiwemo mchungaji wa kanisa hilo.

Maafisa wamelitaja shambulizi hilo kama la uhalifu wa chuki.
Bi Lynch amesema idara ya haki itaangazia maswala yote ili kubaini njia mwafaka ya kumfungulia mashtaka mshukiwa.

Vyombo vya habari vya Marekani vinasema kuwa bwana Storm alikamatwa huko Selby Carolina kaskazini saa 13 baada ya shambulizi.

Mtu wa karibu wa mshukiwa, Dalton Tyler alisema Roof alikuwa akizungumzia kufanya shambulizi kwa kipindi cha miezi sita mfululizo.

"Alikuwa na tabia ya ubaguzi na mambo mengine, alisema ana mpango wa kuanzisha vita kwa kufanya shambulizi na kisha kujiua yeye mwenyewe," Alisema  Tyler.

Mjomba wa mshukiwa, Carson Cowles alisema mwezi wa nne mwaka huu Roof alipewa Pisto kama zawadi ya sherehe ya kuzaliwa.

Alisema licha ya hivyo, familia yao imeshtushwa na tukio hilo lililofanywa na Roof .

"Hakuna aliyejua kama hili lingetokea, kama anahusika na atakamatwa ni lazima aadhibishwe kwa kile alichokifanya," alisema.

Akiongea kuhusu tukio hilo ikulu jana Rais Barack Obama  alilaani kitendo hicho.

alisema, kitendo cha mauaji hayo kufanyika katika kanisa la watu weusi linaamsha maswali kuhusu historia mbaya ya ubaguzi wa rangi Marekani.

Alisema suala hilo linaashara kuwa kuna umuhimu wa kudhibiti matumizi ya silaha.

Chanzo: BBC na Dailymail

No comments:

Post a Comment