KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 19, 2015

SHEIN AAHIDI MAKUBWA AKISHINDA TENA 2015


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohammed Shein amesema mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa asilimia 90 ndiyo uliomsukuma kuchukua fomu ya kugombea tena urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM.
Aidha, ameahidi endapo atapewa tena ridhaa ya kuiongoza Zanzibar katika miaka mitano mingine, atahakikisha Zanzibar inakuwa na maendeleo na mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali, ikiwemo za kiuchumi na utawala bora.
Aliyasema hayo jana alipozungumza na viongozi wa CCM katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui mjini hapa mara baada ya kukabidhiwa fomu ya kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar.
Alifafanua kuwa utekelezaji wa ilani ya CCM na kuwatumikia wananchi kwa uadilifu mkubwa na kuleta maendeleo ndiyo uliomshawishi kugombea nafasi hiyo kwa kipindi cha pili sasa.
“Nimeamua kuchukua fomu kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM kwa sababu ya kupata mafanikio makubwa katika utekelezaji wa ilani ya CCM kwa asilimia 90,” alisema.
Akiyataja baadhi ya mafanikio yake, alisema mara baada ya kuingia madarakani alifanya kazi kubwa kuhakikisha taasisi zinazokusanya kodi zinasimamia majukumu yake ambapo katika mwaka 2011 Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ilikuwa ikikusanya jumla ya Sh bilioni 13.5 na sasa jumla ya Sh bilioni 39 zinakusanywa kwa mwezi.(VICTOR)

No comments:

Post a Comment