KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 23, 2015

POLISI YACHUNGUZA WANNE WALIOMPIGA MGOMBEA URAIS

Dr Kalokola  
                                                                                
Tanga. Jeshi la Polisi limesema lipo katika hatua za mwisho za kukamilisha upelelezi wa tukio la askari wa CCM kumshambulia mtangazania ya urais kupitia chama hicho, Dk Muzzammil Kalokola.
Dk Kalokola alishambuliwa na askari hao , maarufu kwa jina la Green Guard, Juni 17 wakati alipotaka apewe kipaza sauti ili aombe wadhamini kwenye mkutano ambao uliandaliwa kwa ajili ya kumdhamini mgombea mwingine wa urais kwa tiketi ya chama hicho, Edward Lowassa.
Picha za video zilizosambaa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii zinawaonyesha askari hao wakimburuza na baadaye kumpiga ngwala iliyomuangusha chini na mkoba wake ulio na fomu za kuwania urais ukiwa chini.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Zubery Mwombeji alisema jeshi hilo likikamilisha upelelezi litapeleka jalada kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili aweze kutafsiri nguvu iliyotumika kumshambulia na kama waliohusika wanastahili kufikishwa mahakamani.
Mwombeji alitoa taarifa hiyo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limechukua baada ya tukio hilo.
“Tupo katika hatua za mwisho za upelelezi wa tukio la kushambuliwa kwa mtangazania wa CCM. Mwanasheria wa Serikali ndiye mwenye mamlaka kisheria ya kutafsiri na ndiye pia mwenye jukumu la kuamua nini kifanyike,” alisema Mwombeji.
Aliwataja  watu wanne wanaopelelezwa kutokana na kuhusishwa na tukio hilo, akiwamo kiongozi wa kundi la vijana wa CCM wanaojulikana kwa jina la Greenguard na mmoja wa makatibu wa CCM wilayani Tanga ambao majina yao tumesitiri kwa sasa.
Dk Kalokola alishambuliwa wakati alipokuwa akitaka ashughulikiwe kwanza kabla ya mgombea aliyeandaliwa mkutano huo kufika, akidai kuwa ana masuala yanayombana na hasa kesi aliyoifungua ya kupinga mchakato wa Katiba.
Kada huyo alijitetea kuwa alikuwa na miadi na katibu wa CCM siku hiyo na alikuwa anapita kwenye eneo la mkutano.
Dk Kalokola alikiri kupigwa katika tukio hilo lilitokea mchana Jumatano ya Juni 17, 2015 alipofika kwenye ofisi za CCM za Wilaya ya Tanga Mjini.
“Tulielekezwa kuwa makatibu wa CCM wa mikoa ndiyo watakaotutafutia wadhamini siyo sisi tutafute hivyo mimi tarehe 16 nilikwenda ofisi za CCM kuripoti kwa katibu wa Mkoa,” alisema.
Hata hivyo, alisema hakuweza kuonana na katibu huyo baada ya kuambiwa kuwa hayupo na amemwachia majukumu hayo katibu wa CCM wa Wilaya ya Tanga Mjini.

No comments:

Post a Comment