KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 23, 2015

WASSIRA AELEZA SIRI FOLENI YA URAIS CCM

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika,Stephen Wassira                                             
MGOMBEA wa nafasi ya urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wassira amesema kujitokeza kwa idadi kubwa ya wanaoomba nafasi hiyo kwa tiketi ya chama hicho inatokana na ukubwa wa CCM, ambayo ina hazina kubwa ya viongozi.

Akichangia hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2015/2016 bungeni mjini hapa jana kwa kujibu baadhi ya hoja zilizojitokeza wakati wa mjadala, Wassira ambaye pia ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, alisema CCM ni tofauti na vyama vingine ambavyo idadi ya viongozi wao wakishapanda helikopta hakuna mwingine anayebaki chini.
Alisema CCM ni chama kikubwa chenye demokrasia na wala wananchi wasitishwe na idadi kubwa ya wawania urais CCM ambao sasa wanakaribia 40 na kusisitiza kuwa chama hicho kina utaratibu mzuri unaokubalika na wenye kueleweka kwa jamii kuhusu namna ya kupata viongozi.

“Wingi wa wagombea urais ndani ya CCM unatokana na ukubwa wa chama na kukubalika kwake, tofauti na vyama vingine ambavyo viongozi wake wakishapanda helikopta hakuna tena mwingine anayebaki chini,” alisema Wasira.

Pia alieleza kuwa wakati akiwa katika harakati zake za kusaka wadhamini alisafiri kwa siku moja kutoka Songea mkoani Ruvuma hadi Sumbawanga mkoani Rukwa jambo ambalo kwa zamani ilikuwa vigumu na hiyo ni kazi kubwa ya CCM.

Alisema suala la maendeleo ni mchakato na si jambo la siku moja na kushangaa wapinzani kukosoa kwa kudhani maendeleo ni kama mvua na kueleza kuwa baadhi ya mambo yanasemwa na wapinzani sababu huu ni mwaka wa uchaguzi na kudai yatasikika mengi kipindi hiki.
Alieleza kuwa kura hazipatikani kwa mbunge kusemasema bali zinapatikana kutokana na mambo mazuri uliyoyafanya kwa wananchi na kutaja mafanikio mbalimbali ambayo serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais, Jakaya Kikwete imeyafanya.

No comments:

Post a Comment