KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

June 18, 2015

WATU TISA WAUWAWA KATIKA SHAMBULIO LA KANISANI MAREKANI

Reverend Clementa Pinckney
Mchungaji Clementa Pinckney aliyeripotiwa kuuawa kutokana na shambulio hilo.
Tragedy: Local residents and church members embraced and consoled one another in the hours following the incident, the police chief described the incident as a 'senseless, unfathomable' tragedy 
Waumini wa kanisa la AME na watu wa majirani wa eneo la tukio wakiwa katika majonzi baada ya kutokea shambulio hilo.

Shooting: Police responded to the shooting around 9pm at the 150-year-old church and Charleston police chief Gregory Mullen said he believes the shooting was a hate crime
Barabara zikiwa zimefunga kufuatia shambulio lililoua watu tisa kanisani.

Manhunt: A huge manhunt ensued with officers wearing bullet-proof vests and carrying guns; the gunman was still at large at 2am
Askari wakiwa katika harakati za kuimarisha ulinzi eneo la tukio.  
Heartbroken: A man looks on with tears in his eyes as a group of people arrive on the scene to ask about what happened
Kijana akiwa katika hali ya sintofahamu na huzuni kubwa baada ya watu kufika eneo la tukio na kuuliza kilichotokea. 
Prayer Circle: Here, a group of several men are seen standing in a circle in front of a hotel near the church for an impromptu prayer service 
kundi la vijana wakiwa wanasali karibu na eneo la kanisa baada ya tukio la mauaji kutokea.   

 Carolina Kusini, Marekani

POLISI katika jimbo la Carolina Kusini nchini Marekani wamesema mtu mmoja aliyekuwa na bunduki amewapiga risasi na kuwaua watu tisa ndani ya kanisa la Methodist lililoko eneo la Charleston.

Wamesema kwa sasa wanamtafuta mshukiwa huyo anayeaminiwa kuwa kijana wa Kizungu mwenye umri unaokadiriwa kuwa miaka ishirini.

Shambulio hilo limefanyika ndani ya kanisa la Emmanuel African Methodist Church maarufu kama AME, kanisa linaloaminika kuwa la zamani zaidi linalotumiwa na watu wa asili ya Afrika nchini Marekani.

Polisi wamesema kuwa shambulio hilo linatokana na  chuki ya ubaguzi wa rangi  ambapo pia limehusishwa na nguvu ya kisiasa kati ya vyama viwili vya siasa katika eneo la Charleston huko South Carolina kutokana na kile kinachodaiwa kuwa limefanyika saa chache kabla ya Mchungaji Pinckney kukutana na mwendesha kampeni wa Chama cha Democratic cha Marekani, Hillary Clinton, katika sehemu ya kampeni ya kuwania urais wa nchi hiyo. 

Taarifa zinaeleza kuwa mshambuliaji huyo alimtaka mama mmoja wa makamu kuondoka kanisani hapo kabla hajatekeleza azma yake hiyo ya kufanya shambulio hilo.

Lengo la kumwondoa mama huyo lilikuwa ni kumfanya aende akawaambie watu wengine kilichotokea.

Watu wanane walikufa papo hapo na mwingine alifariki akiwa anapata matibabu hosipitali.  Aidha majeruhi mmoja anayeendelea kupata matibabu ameripotiwa kuwa katika hali nzuri.

Mchungaji Pinckney wa kanisa hilo na Seneta wa Jimbo la Carolina Kusini, ni miongoni mwa walioripotiwa kuuawa kutokana na shambulio.

Duru za habari kutoka kwa walioshuhudia tukio hilo zinasema mtoto wa miaka mitano amenusurika kifo kutokana na shambulio hilo baada ya kuambiwa na bibi yake aliyeambatana naye kanisani kuwa aigize kama amekufa mara tu shambulio lilipoanza.

Chanzo: BBC na Dailymail

No comments:

Post a Comment