KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 27, 2015

TUNAHUJUMIWA JAMANI -UKAWA

  Manispaa ya Ilala imesema imezuia uzinduzi wa kampeni za Ukawa Jangwani kwa kuwa siku hiyo kutakuwa na shughuli nyingine ya CCM.
Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia.
Siku chache baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuzindua kampeni za mgombea wake wa urais, Dk. John Magufuli, katika viwanja vya Jangwani, Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam imezuia kuzinduliwa kwa kampeni za mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi  (Ukawa) kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, katika viwanja hivyo.
 
Hatua hiyo imechukuliwa huku Ukawa wakisema wamehujumiwa ili wasizindue kampeni zao keshokutwa.
 
Manispaa hiyo imeeleza kuwa imechukua hatua hiyo kwa kuwa siku hiyo kutakuwa na shughuli nyingine ya CCM.
 
Lowassa ambaye anawakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vya UDP, CUF na NCCR Magezi katika uchaguzi huo, amezuiliwa kuzindua kampeni katika viwanja hivyo kwa madai kuwa uwanja huo utatumiwa kwa shughuli nyingine na CCM.
 
Mwenyekiti mweza wa Ukawa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia, alisema zuio hilo la kutumia uwanja huo limo kwenye barua waliyopelekewa na Manispaa hiyo juzi.
 
“Jambo la kushangaza ni kuwa, awali tuliomba kufanya kampeni zetu uwanja wa Taifa, lakini tukazuiliwa. Sasa tumeomba kuzindulia viwanja vya Jangwani walikofanyia wenzetu wa CCM, lakini pia  tumenyimwa kwa madai kuwa kuna wenzetu wameshaomba kufanyia hapo mkutano, lakini Mgurugenzi wa Ilala ameshindwa kututajia ni chama gani kilicho omba,” alisema Mbatia.
 
Alisema uamuzi huo umewatatiza kwa sababu wanashindwa kuuelewa na kutafsiri kuwa ni  matumizi mabaya ya dola dhidi ya CCM kwa kutumia viongozi na watendaji wake kuzuia kampeni za Ukawa.
 
Mbatia alisema kabla  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, alikaririwa na vyombo vya habari akivitaka vyama vya siasa visivunje taratibu na sheria za uchaguzi.
 
Alisema  pia Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alitoa onyo kwa vyama vya siasa kufuata kanuni na taratibu za kampeni ili kuepuka uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu hadi uchaguzi utakapofanyika
.
“Jambo la kusikitisha na ambalo linatugawa Watanzania, chama dola CCM, kilivunja taratibu hizo kwa kuvuka muda wa kampeni hadi saa moja kasoro usiku badala ya kumaliza saa 12 jioni, pia siku ya uzinduzi, Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, alitumia lugha za matusi, lakini yote hayo yalifumbiwa macho na Nec,” alisema Mbatia.
 
Alisema kanuni na sheria hizo za uchaguzi pia zilivunjwa kwa kuongozwa na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete na kwamba hayo yote wakati yakifanyika Polisi na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Sadiki walikuwa katika viwanja hivyo.
 
MANISPAA YAZUNGUMZIA ZUIO
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mngurumi, alipoulizwa sababu za kuzuia Chadema kuzindua kampeni zake  katika uwanja huo, hakuwa tayari kuzungumzia akidai yuko kikazi mkoani Arusha na kwamba Ofisa Utamaduni wa Manispaa hiyo anakaimu wadhifa wake.
 

No comments:

Post a Comment