KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 8, 2016

ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA KATOLIKI LA DAR ES SALAAM,MUADHAMA,KARDINALI PENGO ARIDHISHWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA KATIKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI(MNH)

jana1
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (kulia) akiwa na Mkuu wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya  Taifa ya Muhimbili (MNH)  jijini Dar es Salaam Profesa Mohamed Janabi alipomtembelea   leo,Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki  la Dar es salaam,Muadhama, Kardinali  Pengo.Picha kwa Hisani ya Wizara hiyo.
MUS2
WAZIRI wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu , akiongozana na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete Profesa Mohamed Janabi wakati alipowasili Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, leo ili kumjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki  la Dar es salaam,Muadhama, Kardinali  Policarp Pengo . Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Mpoki Ulisubisya
MUS1 WAZIRI wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu , akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo, katika taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete,Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, jana. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Mpoki Ulisubisya na katikati ni Dakatari bingwa wa upasuaji wa wa moyo kwa watoto Dk. Godwin Godfrey.

MUS3
WAZIRI wa  Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Ummy Mwalimu , akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa moyo, katika taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete,Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, leo. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo,  Dk Mpoki Ulisubisya na  katikati ni  Dakatari bingwa wa upasuaji wa wa moyo kwa watoto Dk. Godwin  Godfrey.
…………………………………………………………………………………………………
 Na Magreth Kinabo-MAELEZO
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki  la Dar es salaam,Muadhama, Kardinali  Pengo amesema kwamba ameridhishwa na huduma za afya zinazotolewa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), hivyo itakuwa ni vigumu kwa Serikali kumshawishi kwenda kutibiwa nje ya nchi.

Kauli leo na Askofu Pengo ambaye amelezwa katika  Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika hospitali ya  MNH  jiji Dar es Salaam kuanzia  Januari Mosi, mwaka  2016 hadi sasa mara baada ya kuzungumza na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu  ambaye alimtembelea   leo mchana  ili kuweza kufahamu maendeleo ya afya yake.

“Ninapenda kutoa taarifa kwa umma wa Watanzania  na kuwaondoa hofu kuwa hali ya Baba Askofu Pengo imeimarika na  anaendelea vizuri, hajawekewa oxygen wala hajalazwa katika wodi ya uangalizi maalum(ICU) na ameridhika na huduma zinazotolewa.

“Ameridhika  na  huduma zinazotolewa za moyo, itakuwa ni vigumu sisi kama Serikali kumshawishi kwenda kutibiwa nje ya nchi, ” alisema  Waziri huyo.

Aidha Waziri Ummy alitembelea sehemu ya ICU, katika taasisi hiyo, ambapo alisema operesheni ambazo ni ngumu zinafanyika, katika opresheni za moyo kiwango cha kimataifa ni asilimia 6, wakati Tanzania imefikia kiwango cha asilimia 4, hivyo tunafanya vizuri.

Aliongeza kwamba hatua hiyo inapunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi, pia aliwataka hata wagonjwa kutoka taasisi binafsi kwenda kutibiwa katika taasisi hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa taasisi hiyo, Profesa Mohamed Janabi alisema  Baba Askofu huyo ameridhika na matibabu aliyoyapata ambayo yanaweza kufanyika Tanzania, hivyo changamoto iliyopo kwa Serikali kupitia wizara hiyo ni kuiwezesha taasisi hiyo kibajeti ili kuwezesha wagonjwa anagalau 50 kati ya 300 ambao wako kwenye orodha  ya kupatiwa huduma.
Aliongeza kwamba Baba Askofu huyo, ataruhusiwa siku za karibuni, baada ya hali kuendelea vizuri.

No comments:

Post a Comment