
Kutokana na hali hiyo Mhe. Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI ameelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Manispaa ya Ilala kumuondoa kwenye nafasi yake Kaimu Afisa Biashara wa
Manispaa ya Ilala na nafasi yake kukaimiwa na mtu mwingine ili kupisha
uchunguzi zaidi juu ya tuhuma zilizotolewa dhidi yake.
Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
–TAMISEMI amefikia uamuzi huu baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka
kwa Wafanyabiashara ambao wamemlalamikia Mtendaji huyu kwa ukiukwaji wa
Sheria, Kanuni na Taratibu za utoaji wa Leseni za Biashara, Urasimu na
Mazingira ya rushwa.
Katika uchunguzi wa awali uliofanyika kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Ilala mambo yafuatayo yamegundulika:
- Ukiukwaji wa Makusudi wa Sheria, Kanuni na Taratibu za utoaji wa Leseni za Biashara.
- Kutoa Leseni za Biashara zaidi ya 843 bila kuwa na Vyeti vya uthibitisho wa Walipa kodi ‘Tax Clearance Certificates” hivyo kuikosesha Serikali Kodi ya Mapato.
- Kukaa na fomu za Wafanyabiashara 336 kwa muda mrefu bila sababu za msingi.
- Kukiuka Mwongozo wa Mkataba wa Huduma kwa wateja ambao unamtaka Afisa Biashara kutoa Leseni za Biashara ndani ya siku 2 hadi 3 baada ya muombaji kuwasilisha maombi yake ya kupatiwa Leseni ya Biashara.
Aidha, Mheshimiwa Waziri wa Nchi ,
Ofisi ya Rais-TAMISEMI amewaagiza Maafisa Biashara wote nchini watoe
huduma za Leseni kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu , kuacha
urasimu na kujiepusha na vitendo vya rushwa.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi ya Rais-TAMISEMI,
07 Januari, 2016.
No comments:
Post a Comment