
Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo (mbele katikati), akiongea jambo wakati wa
kikao kati yake na wawekezaji katika Sekta ya Nishati, katika Ukumbi wa
Tanesco, Jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi wa Kituo
cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Julieth Kairuki.
Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo, akiongea jambo na baadhi ya wawekezaji mara
baada ya kikao chake na wawekezaji ambao wameonesha nia kuwekeza katika
vyanzo mbali mbali vinavyopatikana nchini na baadhi wamefika kupata
taarifa kuhusu uwekezaji.
Baadhi ya Watendaji kutoka
Taasisi zilizo chini ya Wizara na Maafisa kutoka Wizarani wakifuatilia
kikao kati ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo na Wawekezaji
katika Sekta ya Nishati,
Baadhi ya Wawekezaji
wakiwasilisha taarifa zao za uwekezaji kwa Waziri wa Nishati na Madini
Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani). Baadhi ya maswali ambayo
Profesa alihoji kutoka kwa wawekezaji hao wao ni uwezo wao kifedha,
kiteknolojia,utaalam na uzoefu wa kazi katika vyanzo walivyochagua
kuwekeza nchini.





No comments:
Post a Comment