
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongea na Vyombo
mbalimbali vya Habari mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa nane wa
Mifuko ya Jamii Afrika Mashariki na Kati. Mkutano huo wa siku mbili
unafanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti,
Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa NHIF Rehani Athumani akifuatilia mkutano
wa Umoja wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Afrika Mashariki uliofanyika
leo Jijini Dare s salaam.

Baadhi ya washiriki waliohudhuria
mkutano wa vyama vya mifuko ya Jamii Afrika Mashariki na kati wakiwa
wamesimama kumuaga mgeni rasmi Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu Hassan
alipokuwa akifungua mkutano huo leo Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais Mhe.Samia Suluhu
Hassan akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya mawaziri na manaibu
waziri kutoka nchi mbalimbali za Afrika ya Mashariki na Kati wakati wa
mkutano wa Umoja wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Afrika Mashariki na kati
leo Jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikabidhi cheti katika
Mkutano wa Nane wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Afrika Mashariki na Kati.
Makamu wa Rais amefungua rasmi mkutano huo leo katika Ukumbi wa Benki
Kuu.


No comments:
Post a Comment