
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia aliyevaa kiraia)
akiingia ndani ya Kiwanda cha Viatu Gereza Karanga mjini Moshi.
Rwegasira amefanya ziara kwa kukitembelea kiwanda hicho kwa lengo la
kujifunza shughuli mbalimbali zinazofanywa na Jeshi la Magereza. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto) akimsalimia
Mkuu wa Magereza mkoani Kilimanjaro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Magereza, Venant Kayombo wakati Kiongozi huyo wa Wizara alipowasili
katika ofisi za Magereza Mkoa, mjini Moshi.
Fundi wa Kiwanda cha Viatu Gereza
Karanga mjini Moshi, Hashim Rashid akimuonyesha Katibu Mkuu wa Wizara
ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kushoto)
jinsi buti la Jeshi linavyotengenezwa ndani ya kiwanda hicho.




No comments:
Post a Comment