KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 1, 2016

FAHAMU MENGI KUTOKA UTT-PID



Ofisa Mtendaji Mkuu wa  UTT-PID  Dkt. Gration Kamugisha
Katika kuhakikisha kwamba taifa linapiga hatua kubwa ya kimaendeleo na wanachi wanapata huduma bora na kwa wakati Serikali imeanzisha taasisi mbalimbali za umma mojawapo ya taasisi  hizo ni UTT-PID.
UTT –PID, Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu  (UTT-Projects  and Infrastructure Development  ) ni taasisi ya Serikali iliyo chini ya Wizara ya Fedha ambayo ilianza shughuli  zake rasmi Julai Mwaka  2013 .
Ofisa Mtendaji Mkuu wa  UTT-PID  Dkt. Gration Kamugisha anasema kuwa taasisi hiyo  inamilikiwa na Serikali ya  Jamhuri ya Muungano kwa asilimia mia moja.
Anazitaja kazi  kuu za UTT-PID kuwa ni utoaji wa huduma za  ushauri katika maeneo ya Upembuzi yakinifu wa miradi mbalimbali,maandalizi ya hadidu za rejea’,mipango ya huduma za kifedha , kuwasilisha miradi na huduma zinazohusiana.
 Msingi wa kuanzishwa kwa taasisi hii na Serikali ni kuweka manzingira wezeshi ili kupata au kuvutia mtaji binafsi (private capital)  katika kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo sharti iwe inakidhi vigezo vya kuwa na faida za kijamii, kiuchumi na kifedha.
Miradi mingi iliyotekelezwa hadi sasa inahusiana na  uendelezaji wa ardhi na majengo  lakini  lengo na mtazamo wa taasisi ni zaidi ya hapo. Ipo miradi mingi na mikubwa ya kimiundombinu katika sekta za afya, elimu, nishati, nk ambayo imeletwa kwenye taasisi na wadau mbalimbali hasa taasisi za umma ambayo inatafutiwa fedha
Dkt. Kamugisha anafafanua kuwa ili taasisi yoyote ile ipige hatua ni lazima iwe na Dira hivyo kwa upande wao Dira yao ni kuwa mdau wa maendeleo  wa kuaminika katika fani ya Usimamizi wa Miradi na Maendeleo ya Miundombinu na kuwa na mtazamo wa uwajibikaji wa dhati ili kutosheleza mahitaji kwa wateja na kuendelea kuboresha huduma.
“Lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunawajibika kwa wateja watu.. na katika hili ni lazima tutoe huduma bora mbazo zinakata kiu ya wateja wetu” anasema. 
Itaendelea Jumatatu....

No comments:

Post a Comment