
Mkurugenzi Mtendaji, wa Chuo cha 
Jemolojia  cha Madagascar, Rasolonjatovo Adrianirina  akizungumza na 
Washiriki wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito- Arusha yaliyoanza 
 jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
Kamishna Msaidizi wa Madini, 
Kanda Kusini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka akizungumza wakati wa Semina 
ya Mafunzo kutoka Chuo cha Jemolojia cha Madagascar iliyotolewa wakati 
wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito- Arusha yaliyoanza  jijini 
Arusha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa 
Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), Mhandisi Dominic Rwekaza (kushoto) 
akiwa na Meneja Mradi wa Usimamizi Endelevu wa  Rasilimali Madini 
(SMMRP), Mhandisi  Idrisa Yahaya na Kiongozi wa Mradi     wa SMMRP wa 
Benki ya Dunia, Mamadou Barry       wakizungumza mara baada ya 
kuhudhuria  Semina ya Mafunzo kutoka Chuo cha Jemolojia cha Madagascar 
iliyotolewa wakati wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito- Arusha 
yaliyoanza  jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
Mjiolojia kutoka Idara ya Madini,
 Asimwe Kafrika akizungumza wakati Semina ya Mafunzo kutoka Chuo cha 
Jemolojia cha Madagascar iliyotolewa wakati wa Maonesho ya Tano ya 
Kimataifa ya Vito- Arusha yaliyoanza  jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 
Aprili, 2016.
Washiriki wa Maonesho ya Tano ya 
Kimataifa ya Vito- Arusha yaliyoanza  jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 
Aprili, 2016 wakiwa katika Semina ya Mafunzo kutoka Chuo cha Jemolojia 
cha Madagascar iliyotolewa wakati wa Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya 
Vito- Arusha yaliyoanza  jijini Arusha tarehe 19 hadi 21 Aprili, 2016.
……………………………………………………………………………………………………………..
Na Asteria Muhozya, Arusha
Imeelezwa kuwa, Serikali imeandaa
 mpango wa  kuhakikisha inakiendeleza Kituo Cha Jemolojia Tanzania (TGC)
 ili kiwe kituo Bora cha utoaji mafunzo ya uongezaji thamani madini 
nchini.
 Hayo yameelezwa na Meneja Mradi 
wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP), Mhandisi Idrisa 
Yahaya katika Maonesho ya Tano ya Kimataifa ya Vito yaliyofanyika jijini
 Arusha kuanzia tarehe 19 hadi 21, Aprili, 2016.
Mhandisi Yahaya aliyasema hayo 
baada ya kuhudhuria semina ya mafunzo kuhusu madini ya Vito na  uzoefu 
yaliyotolewa na Wataalam waliobobea kwenye Sekta hiyo kutoka nchi ya 
Madagasca wakati wa Maonesho hayo.
Mhandisi Yahaya alisema kuwa, 
bado jitihada zinafanywa na Serikali kuwekeza zaidi katika Kituo hicho 
jambo litakalopelekea kufikia kiwango ambacho nchi ya Madagasca imefikia
 katika utoaji mafunzo mbalimbali katika sekta hiyo.
Aliitaja mipango hiyo kuwa ni 
pamoja na upatikanaji wa wakufunzi kutoka nje ya Tanzania, kukiunganisha
 Kituo cha TGC na vituo vingine  vya kimataifa duniani na ununuzi wa 
vifaa vya mafunzo.
“ Bado tunahitaji kuwekeza zaidi 
katika Chuo chetu ili kuweza kufikia hatua iliyofikia nchi ya Madagasca.
 Kuna mipango mingi imeandaliwa kwa ajili ya kituo hicho,” alisema 
Mhandisi Yahaya.
Kwa upande wake, Mratibu wa Kituo
 cha TGC, Musa Shanyangi akieleza mipango ya kituo hicho  mara baada ya 
kuhudhuria semina hiyo alisema ni pamoja na kuanzisha  kozi  ya 
Jemolijia, usonara, kuongeza idadi ya wanafunzi  wanaosoma  kozi  ya lapidary kutoka
 wanafunzi 18 wa sasa hadi wanafunzi 36, kuanzisha maabara ya utambuzi 
wa madini ya vito na kuanzisha makumbusho ya madini ya vito na bidhaa za
 usonara.
Akiwasilisha uzoefu wa  Chuo cha 
Jemolojia cha nchini Madagasca (IGM) wakati  akitoa  mada kuhusu chuo 
hicho kwa washiriki wa maonesho hayo,  Mkurugenzi Mtendaji, 
Rasolonjatovo Adrianirina alieleza kuhusu mafunzo na huduma mbalimbali 
zinazohusu Chuo hicho ambacho  kinatajwa kuwa Chuo bora  kwa utoaji wa  
mafunzo ya aina mbalimbali katika fani za Jemolojia Afrika.
Alisema kuwa, mafunzo 
yanayotolewa na Chuo hicho yapo katika vipindi tofauti kulingana na aina
 ya mafunzo yanayotolewa na hivyo kuwataka washiriki kuona umuhimu wa 
kukitumia chuo hicho kupata mafunzo kwa lengo la kuwezesha uongezaji 
thamani wa madini katika nchi husika.
Kituo cha Jemolojia Tanzania 
(TGC), cha jijini Arusha, kilianzishwa ikiwa ni moja ya hatua  za 
Serikali za kutimiza malengo yaliyomo katika Sera ya Madini ya Mwaka  
2009 yenye lengo la kuongeza  mchango wa Sekta ya Madini katika pato la 
Taifa na ajira kwa Watanzania kupitia Uongezaji thamani madini hapa 
nchini.
Aidha, mafunzo yanayotolewa na 
Kituo hicho ni pamoja na ukataji na ung’arishaji wa madini ya Vito ( 
Lapidary), utengenezaji wa  bidhaa za mapambo,  (Jewelry Design and 
Manufacturing) na uchongaji wa vinyago vya mawe  (Stone Carving).
Uongezaji thamani madini unalenga
 kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania watakaofanya kazi kwenye vituo 
vya kuongeza thamani madini huku wengine wakijiajiri na kuongeza mapato 
ya Serikali, hivyo kuongeza mchango wa Sekta ya Madini katika Pato la 
Taifa.
Kituo cha Jemolojia  kilianzishwa na Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Dunia.






No comments:
Post a Comment