KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 4, 2016

KUTOKA UTT-PID


Ofisa Mtendaji Mkuu wa UTT-PID,Dkt.Gration Kamugisha

Ijumaa iliyopita tuliangazia historia ya UTT-PID, leo Ofisa Mtendaji Mkuu Dkt.

Gration Kamugisha anaelezea zaidi majukumu mbalimbali ya taasisi yake ...ungana naye.
 Anabainisha kwamba Dhamira yao ni kufungua mitaji iliyodumaa kwa kuwasaidia wateja kitaalam  katika maeneo ya  miradi na maendeleo ya miundombinu  na kuleta ukuaji wa mapato kwa ajili ya wateja na wadau ambao ni pamoja mwanahisa (serikali). .

“Na katika kutekeleza hilo kuchochea ukuaji wa uchumi na huduma za kijamii katika sehemu husika ambayo sisi tunahusisha mitaji iliyo lala,” anasema.
Anasema kwamba mfano wanapokwenda kupanga mji katika eneo lolote katika nchi yetu, ni wazi kamba barabara zitachongwa, huduma za umeme zitafika, huduma za maji zitakuwepo, na shughuli nyingine za kiuchumi zinazoendana na huduma hizo zitafanyika,”
“Kwa hiyo utaona ni dhahiri kwamba wananchi watafaidika na huduma zinzotokana na uwezekezaji wetu katika eneo husika na hivyo kuchangia ukiuaji wa uchumi,” anasema.
Lakini pia Dkt. Kamugisha anasema katika kufanikisha yote hayo ni lazima kuwe na maadili , hivyo suala la maadili kwao ni kipaumbele pia .
“Tunaongozwa na misingi ya uwajibikaji, uwezo na  motisha kwa wafanyakazi , uhakika wa  ongezeko la wafanyakazi wenye sifa ,kuthamini uvumbuzi ,utambuzi na  maboresho ili kuepuka au kupunguza uwezekano wa kujitokeza kwa malalamiko”.
Pia katika kuteleleza majukumu yao anasema suala la ubora wa huduma ni kipaumbele
“Kutekeleza dhana nzima ya utoaji bidhaa /huduma zenye sifa na thamani ya kipekee huku wakihakikisha kwamba  gharama nafuu kwa kujitahidi katika kuboresha huduma na bidhaa zao” anasema.
Anabainisha kuwa wamekuwa wakijitahidi kutoa huduma bora kwa wateja wao katika kuhakikisha kwamba wanafanya kazi kulingana na thamani ya fedha na hivyo kumridhisha mteja.
“Tunajitahidi sana kukidhi  mahitaji ya mteja,  kuhakikisha kwamba taasisi inatoa huduma zilizo bora kwa wateja wao  kwa kiwango kinachokidhi na hata kuzidi matarajio yao,”.
Kuhusu suala la faida anasema kwamba taasisi yake imejikimu kimsingi katika uwezo wa kuongeza faida kutokana na uwekezaji wake kama vile....
Itaendelea kesho

No comments:

Post a Comment