KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

May 18, 2016

MALIASILI NA UTALII KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUWEKEZA KATIKA UTALII WA KUSINI MWA TANZANIA

index
Na Tiganya Vincent-MAELEZO_Dodoma.
Wizara ya Maliasili na Utalii imesema kuwa inatarajia kuboresha utalii wa kusini mwa Tanzania kupitia miradi mbalimbali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo chini ya mradi wa REGROW unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama za shilingi  bilioni 2.1.
Fedha hizo zinafadhiliwa na Benki ya Dunia  sawa na Dola za Kimarekani zisizopungua milioni moja.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Injinia Ramo Makani wakati akijibu swali Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini Mhe. Hassan Kaunje aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuendeleza utalii wa ukanda wa kusini.
Alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuwekeza katika miundombinu ya utalii kwa ajili ya kuutangaza utalii wa Ukanda wa Kusini mwa Tanzania ili uweze kusaidia ukuaji wa uchumi na ustawi wa Taifa.
Alisema kuwa mpango huo utajumuisha kuimarisha mafunzo ya utalii na kutenga maeneo maaalum ya utalii katika fukwe za bahari na maziwa kwa ajili hoteli za kitalii.
Mhe. Makani alisema kuwa Serikali imepanga kutekeleza mkakati wa kuutangaza maeneo ya utalii ikiwemo vivutio kihistoria na kiutamaduni kama vile mji wa kihistoria wa Mikindani, Kilwa Kivinje, Pori la Akiba Lukwika-Lumese na Pori la Akiba la Seleous.
Aliongeza kuwa ili kukuza utalii wa fukwe katika eneo hilo , Serikalai imejipanga kutenga maeneo maalum hususan kwa ajili ya hoteli za kitalii kando ya Bahari ya Hindi mkoani Mtwara na Lindi.

No comments:

Post a Comment