![]() |
Utafiti ulofanywa mwaka 2009 na
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali wa masuala ya watoto hapa nchini ulionyesha kuwa kuna
kiwango kikubwa cha ukatili dhidi ya watoto.
Hata hivyo, pamoja na kuwa ni
utamaduni wa kigeni kuripoti matukio mbalimbali kupitia namba za simu na
kwenye mitandao, matumizi ya namba 116 (Child helpline) hapa nchini
yamesaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa taarifa za ukatili dhidi ya
watoto.
Kama anavyoeleza Mkurugenzi
Msaidizi wa Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na Watoto, Bwana. Benedict Missari kuanzia mwezi Juni 2013 hadi
mwezi Juni 2014, Wizara hiyo ilipokea jumla ya simu 16000 kati ya
hizo1659 zilielezea ukatili dhidi ya watoto.
Kati ya simu hizo 1659, “simu 107
zilikuwa za ‘physical violence’, 23 za ubakaji, 23 za unyanyasaji
mwingine wa kingono, 69 ni za kutelekezwa, 6 za utekwaji wa watoto, 12
zilihusu mimba kwa watoto huku 21 ni za uuzwaji wa watoto kwenda maeneo
mbalimbali mfano Zanzibar na nchi za Uarabuni”.
Watoto walio na umri wa chini ya miaka 18 nchini Tanzania ni sawa na asilimia 51 ya jumla ya idadi ya wananchi wote nchini.
Matukio mengi ya ukatili dhidi
yao yamekuwa yakifanyika ama shuleni au nyumbani yakiwemo ya kubakwa,
kukeketwa, kutelekezwa, kuchomwa moto, kutumikishwa kazi chini ya umri
mdogo pamoja na ukatili mwingine wa aina hizo ambao huathiri maendeleo
ya mtoto.
Ili kukabiliana na hali hiyo,
mnamo tarehe 3 Januari, 2013 Serikali chini ya Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto kwa kushirikiana na Asasi isiyokuwa ya
Kiserikali ya C-Sema chini ya Child Helpline International(CHI)
ilianzisha na kuendesha mtandao wa mawasiliano ya simu katika maeneo ya
majaribio (Pilot Areas) katika wilaya sita ambazo ni Wilaya/Manispaa za
Temeke, Magu, Bukoba Vijijini, Musoma Mjini, Kasulu na Hai ili kupata
taarifa za ukatili wa watoto kwa kupiga simu bure kwa kutumia namba
116(Child helpline).
Mtandao huo wa mawasiliano
unatoa fursa kwa watoto na au watu wazima kwa niaba ya watoto kutoa
taarifa za ukatili unaofanywa kwa watoto katika eneo fulani ili
kuwezesha wahusika kufuatilia kwa karibu na kutoa msaada kwa
mtoto/watoto waliofanyiwa vitendo vya ukatili kwa kuwachukulia hatua
wahusika wa vitendo hivyo vya ukatili.
Kupokelewa kwa taarifa ukatili
dhidi ya watoto kumeweza kufanyiwa kazi kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali ikiwemo makampuni ya simu kwa kumwezesha mtoa taarifa kupiga
simu hiyo bure, Polisi kwenda kukamata wahusika na kuwafikisha sehemu
husika kulingana na Sheria na taratibu za nchi, na hospitali kutoa
huduma kwa wahusika wa matatizo mbalimbali yanayohitaji huduma za
kiafya.
|
May 13, 2016
MATUKIO MENGI YA KIKATILI DHIDI YAO YAMEKUWA YAKIFANYIKA AMA SHULENI AU NYUMBANI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)



No comments:
Post a Comment