KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 24, 2016

KIJANA ALIYEENDA KUSOMA UJERUMANI, AITUMIA FURSA HIYO KUSAKA WAWEKEZAJI NCHINI

1
Kijana Petro Magoti kutoka Shirikisho la Vyuo vya Elimu ya Juu-CCM,  aliyeko Ujerumani kwa masomo ya Uongozi na Uhusiano wa Kimataifa, akiagana na mmoja wa wamiliki wa viwanda vikubwa Duniani, Prof. Karl Knoop, baada ya kuzungumza naye,  mjini Berlin, Ujerumani, juzi. Kushoto ni Meya  wa mji wa Bugermeister, David Osthotlhoff.
NA BASHIR NKOROMO Katika kutekeleza azma ya Serikali ya awamu ya tano ya kuifikisha Tanzania katika mapinduzi ya viwanda vikubwa na Vidogo, Kijana Petro Magoti ambaye ni mwakilishi pekee kwa Tanzania aliyeko nchini Ujerumani, kwenye mafunzo ya uongozi na uhusiano wa kimataifa, amekutana na mmoja wa wamiliki wa viwanda vikubwa Duniani, Prof. Karl Heinz Knoop na kufanya mazungumzo naye ili kumshawishi kuja kuwekeza nchini.
Akizungumza kutoka nchini Ujerumani, Magoti amesema leo kwamba, Prof. Knoop ambaye anamiliki viwanda katika nchi 17 Barani Ulaya na katika nchi nne katika bara la Afrika, katika mazungumzo yao, Prof. Knoop ameonyesha dhamira ya kuwekeza Tanzania katika meneo ya Himo mkoani Kilimanjaro na Kilindi mkoani Tanga.
Magoti amesema, Prof, Knoop, amefikia dhamira hiyo baada ya kumweleza kwa kina fursa za kiuchumi zilizopo Tanzania, na namna nchi ilivyojipanga kuwapokea kwa ukarimu wawekezaji kutoka nchi za nje ikiwemo Ujerumani, lengo likiwa kuifikisha nchi kuwa yenye viwanda na hivyo kuwezesha wananchi wengi wakiwemo vijana kupata ajira za uhakika.
“Katika mazungumzo yetu, Prof. Karl Heinz Knoop ameeleza kuwa na dhamira ya kuwekeza Tanzania ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuondoa umasikini, hata hivyo akasema, awali amewahi kuonyesha azma hiyo kwa wakati, lakini akakumbana na changamoto lukuki ikiwemo kupewa eneo la kujenga viwanda vikubwa vya mashine za kilimo kama vile Matrektar, Mashine za kupanda mbegu, Kuvuna na kukausha mazao, na Maghala makubwa ya kuhifadhia vyakula na kiwanda cha magari makubwa ya mizigo”, aalisema Petro.

No comments:

Post a Comment