Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar
Naibu Waziri wa Afya Harusi
Said Suleiman amesema hapendelei kuona wauguzi wanatumbuliwa majipu
kutokana na uzembe wao lakini hayuko tayari kutumbuliwa yeye kwa ajili
yao .
Hayo aliyasema wakati alipokuwa
akifanya ziara ya kutembelea vituo mbali mbali vya Afya Wilaya ya
Kaskazini B Unguja vikiwemo Kituo cha Kiwengwa na Kituo cha Bubwini
Misufini kutaka kuona changamoto zinazopo vituo hapo.
Alisema kuna baadhi ya wauguzi
huwafanyia dharau wagonjwa au wajawazito wakati wa kujifungua jambo
ambalo halipaswi kuona linafanyika, kitu ambacho kinaweza kuwapeleka
pabaya na kutumbuliwa majibu.
“Sitoona vizuri kuona mfanyakazi
anatumbuliwa jipu kwa ajili ya uzembe wake na pia siko tayari
kutumbuliwa mimi kwa ajili yake “Alisema Harusi .
Aidha alisema kwamba wauguzi
wawetayari kukamilisha majukumu yao ya kikazi na waache lugha chafu
ambazo zitawasumbuwa wagonjwa na kuonekana kuwa wao wakorofu katika
kutoa huduma .
Hata hivyo Naibu Waziri alieleza
kuwa wauguzi waelewe kuwa awamu iliopo hivi sasa ni awamu ya
uwajibikaji na ufatiliaji na ni rahisi mawasiliano kufika kwa haraka na
kuweza kuharibu malengo ya baadae hivyo wasiwe tayari kuchokozwa
wakachokozeka.
Nae Muuguzi wa kituo cha afya cha
Kiwengwa Khadija Ali Juma alieleza matatizo mbali mbali ambayo
wanakabiliana nayo kituoni hapo ikiwemo kutokuwa na uzio katika eneo
hilo, wananchi kuchafua katika kwa makusudi katika maeneo ya vyoo pamoja
na kufanya maskani katika kituo hicho .
Aidha alisema kutokuwa na friji
katika kituo hicho kunachagia usumbufu mkubwa wa kuhifadhia dawa za
chanjo za mama na watoto ambazo zinahitajika kuhifadhiwa katika sehemu
yenye ubaridi ili zisiharibike .
Alisema ushirikiano mdogo uliopo
baina ya kituo cha afya na kamati ya sheha hawaufurahikii wauguzi ,kwani
sheha wa sehemu hiyo haonyeshi ushirikiano mzuri na wauguzi waliopo
katika kituo hicho .
Wakati huo huo Naibu Waziri wa
Afya alitembelea katika Kituo cha Afya cha Bumbuni Misufini ambacho
kilitokezea matatizo ya kutofahamiana kati ya Wauguzi wa serikali na
Wakunga wa Jadi .
aliwataka wauguzi ambao ni
waajiriwa wa serikali kutoa mashirikiano ya pamoja na wakunga wa jadi
ili kuepusha tofauti miongoni mwao na kuweza kutatua changamoto ambazo
zitaweza kujitokeza kwa wazazi .
No comments:
Post a Comment