KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

August 20, 2016

SIMBA YAIBAMIZA NDANDA FC YA MTWARA MAGOLI 3-1 LIGI KUU UWANJA WA TAIFA

TAI1
Mchezaji wa timu ya Ndanda FC ya Mtwara akikokota mpira huku mchezaji wa Simba Laudit Mavugo akimfukuzia katika mchezo wa Ufunguzi wa Ligi Kuu ya Vodacom kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jioni hii . Timu zote zimepata magoli katika kipindi cha kwanza Simba ikijipatia  goli lake  kupitia kwa Laudit Mavugo huku Ndanda FC ikisawazisha kupitia mchezaji Omary Mponda.
Katika kipindi cha pili wachezaji wa timu ya Simba Fredrick Blagnon na Shiza Kichuya wamefanikiwa kuifungia timu yao magoli mawili na kuifanya Simba kushinda mchezo huo 3-1 dhidi ya Ndanda FC.
1
Mchezaji wa Fredrick Magnon akiruka juu na golikipa wa timu ya Ndanda FC Jackson Chove huku wachezaji wa timu hiyo wakiangalia wakati mchezo huo wa ligi kuu unaendelea.
2
Wachezaji wa Ndanda FC na SimNdanda ba wakiwania mpira golini mwa lango la FC.
3
Mashabiki wa timu ya Simba wakishangilia kwa nguvu mara baada ya timu yao kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya Ndanda FC.
TAI2
Mashabiki wa timu ya Ndanda FC wakiishangili timu yao wakati ikimenyana na timu ya Simba ya Dar es salaam kwenye uwanja wa Taifa jioni hii.
TAI3
Mashabiki wa timu ya Simba wakionyesha kumlaumu mwamuzi hayupo pichani kutokana na baadhi ya maamuzi katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment