KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 31, 2016

AZAM NJOONI :TOTO AFRICAN

_mg_9761
Na.Alex Mathias,Dar es salaam.
Baada ya kupata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa CCM Kirumba Mwanza timu ya Toto African ‘Wana-kisha mapanda’ wametuma salama kwa wana rambaramba Azam Fc mchezo wao utakaopigwa Jumatano hiii.
Akizungumza Ramadhani Aiko,ametamba kuwa wana imani kuwa watashinda mechi hiyo kutokana ushindi wa Mtibwa kuwapa morali wachezaji pamoja na benchi nzima la ufundi huku wakichangizwa na uwepo wa mashabiki.
“Tunajipanga kuchukua alama tatu muhimu katika mchezo wetu na Azam hivyo tuna tuma salama mapema kuwa wajiandaa kula kichapo kwani tulianza kufunga na Mtibwa goli mbili hata hivyo vijana walijipanga na kupigana na kurudisha na kupata ushindi wa 3-2″alisema Aiko
Toto walitoka nyuma ya kufungwa magoli mawili na wakata miwa na waliporudi walikuja kupigana na hatimaye kushinda hivyo mchezo utakuwa mkali na wa upinzani kwa timu zote mbili ukiangalia hata Azam nao wametoka kushinda magoli 3-2 dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa Kaitaba.
Kwa upande wa Msemaji wa Azam Jafar Maganga,ametamba kuwa nia yao ni kupata alama tatu na malengo yao ni kuchukua pointi zote tisa wakiwa kanda ya ziwa na mchezo na Toto watashinda japokuwa sio rahisi.
“Tumejipa kuwafunga Toto wakiwa hapo kwao kama tuliweza kupata ushindi dhidi ya Kagera hivyo tunajua wapinzani wetu wanacheza vipi na wakiwa nyumbani wanaonekana wangumu mpira ni dakika 90 sisi tumejiandaa kushinda tunasubiri siku ifike tu”alisema Maganga
Azam Fc wanakutana na Toto wakiwa nafasi ya nne wakiwa na alama 19 wakati Toto wao wapo nafasi ya 15 na alama zao 11.

No comments:

Post a Comment