KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 3, 2016

JENGO LA CWT PWANI ,LAIBIWA COMPUTER 11 NA ZAIDI YA MIL.5

cwt
Katibu wa chama cha walimu mkoani Pwani, (CWT),Nehemiah Joseph ,akizungumza kuhusiana na wizi uliotokea katika jengo la  chama hicho ,ambapo computer za mezani na mpakato 11 zimeibiwa na zaidi ya mil.5 .(picha na Mwamvua Mwinyi).
………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
OFISI sita zilizopo jengo la chama cha walimu mkoani Pwani(CWT)zimevunjwa na kuibiwa Kompyuta za mezani na mpakato 11 zinazodaiwa kufikia sh.mil 15 na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.
Mbali ya kuibiwa vitendea kazi hivyo,watu hao pia wamechukua kiasi cha fedha taslimu sh. mil 5,036,515 zilizokuwepo katika baadhi ya ofisi hizo.
Kufuatia tukio hilo, jeshi la polisi mkoani Pwani,linawashikilia walinzi wawili wa jengo hilo kutoka kampuni ya Noble security Tanzania ltd ya Kibaha,Hamad Kisoki(32)mkazi wa Mailmoja na Said Mohammed (39) mkazi wa Mwanalugali.
Akizungumzia kuhusiana na tukio hilo,katibu wa CWT mkoani humo,mwl Nehemiah Joseph,alisema tukio limetokea usiku wa octoba mosi kuamkia octoba 2 mwaka huu.
Alisema siku ya tukio walinzi waliotakiwa kuingia kazini walikuwa ni wawili lakini badala yake aliingia mmoja ambae ni Said Mohammed .
“Ambapo alipokuwa kwenye lindo anadaiwa kupatiwa chips na kinywaji aina ya juise vinavyosemekana kuwa na madawa ya kulevya kutoka kwa mwanamke asiyefahamika”.alisema

No comments:

Post a Comment