
Katibu wa chama cha walimu mkoani
Pwani, (CWT),Nehemiah Joseph ,akizungumza kuhusiana na wizi uliotokea
katika jengo la chama hicho ,ambapo computer za mezani na mpakato 11
zimeibiwa na zaidi ya mil.5 .(picha na Mwamvua Mwinyi).
………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
OFISI sita zilizopo jengo la
chama cha walimu mkoani Pwani(CWT)zimevunjwa na kuibiwa Kompyuta za
mezani na mpakato 11 zinazodaiwa kufikia sh.mil 15 na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.
Mbali ya kuibiwa vitendea kazi
hivyo,watu hao pia wamechukua kiasi cha fedha taslimu sh. mil 5,036,515
zilizokuwepo katika baadhi ya ofisi hizo.
Kufuatia tukio hilo, jeshi la
polisi mkoani Pwani,linawashikilia walinzi wawili wa jengo hilo kutoka
kampuni ya Noble security Tanzania ltd ya Kibaha,Hamad Kisoki(32)mkazi
wa Mailmoja na Said Mohammed (39) mkazi wa Mwanalugali.
Akizungumzia kuhusiana na tukio
hilo,katibu wa CWT mkoani humo,mwl Nehemiah Joseph,alisema tukio
limetokea usiku wa octoba mosi kuamkia octoba 2 mwaka huu.
Alisema siku ya tukio walinzi
waliotakiwa kuingia kazini walikuwa ni wawili lakini badala yake
aliingia mmoja ambae ni Said Mohammed .
“Ambapo alipokuwa kwenye lindo
anadaiwa kupatiwa chips na kinywaji aina ya juise vinavyosemekana kuwa
na madawa ya kulevya kutoka kwa mwanamke asiyefahamika”.alisema


No comments:
Post a Comment