KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 30, 2016

KAGERA SUGAR TUNA IMANI NA KOCHA MECKY MEXIME,MASHABIKI TULIENI.

10
Na.Alex Mathias.
Uongozi wa timu ya soka ya Kagera Sugar umesema kwamba bado una inami na kocha mkuu wa klabu hiyo Mecky Mexme licha ya baadhi ya mashabiki kuonyesha mabango ya kutokuwa na imani nae ya kuendelea kusalia ndani ya kikosi cha timu hiyo.
Mwenyekiti wa Kagera Sugar Salum Madaki, amesema kuwa kwanza anashangazwa na mashabiki wa timu hiyo kudiriki kubeba mabango ambayo hayana msingi kwani kwa hali ilivyo  kocha wao anastahili kupewa sifa kwa jitihada kubwa alizozifanya za kuhakikisha timu bado ipo katika nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi tofauti na msimu uliopita.
Madaki amesema kuwa mashabiki wa timu hiyo wasigetemee kuondoka kwa Mexme ndani ya kikosi hicho kwa wakati huu kwani uongozi bado unaridhishwa na ufundishaji wake licha ya kupoteza michezo miwili mfululizo ikiwemo dhidi ya Azam ambapo walikubali kufungwa kwa jumla ya mabao 3-2 huku wakiwa wametoka kufungwa na Yanga mabao 6-2. Na Mpaka sasa Kagera Sugar ipo nafasi ya tano wakiwa na alama 18 na tofauti na Msimu uliopita kwani ilijinasuwa kushuka daraja hivyo mashabiki watulie kwani Mexime ni kocha bora hapa nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment