KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 7, 2016

MADEREVA WA MAGARI YABEBAYO MCHANGA WAITISHIA TANROADS PWANI

Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MADEREVA wa matipa ya mchanga ,wanaotumia barabara kuu ya Dar es salaam –Morogoro, wamefanya mgomo baridi ,kulalamikia wakala wa barabara (TANROADS)mkoani Pwani,unaowakamata kutokana na kutofunga mchanga vizuri na kuwapiga faini ya sh.500,000.
Madereva hao waliweka mgomo huo katika eneo la Tamco ambapo ndipo watendaji wa wakala huo walikuwa wakiwasimamisha kwa ajili ya kukagua wale waliojaza mchanga hali inayosababisha kuchafua miundombinu ya barabara.
Dereva Martine Magari na Emmanuel Shao,walisema ni kweli wapo madereva wasiofunga vizuri maturubai ya magari yao lakini tatizo kubwa ni kukosa elimu ya kufunga kwa ubora .
Shao aliziomba idara ama mamlaka husika kutoa elimu juu ya sheria mbalimbali kwani inakuwa sio rahisi kuelewa sheria zote zinazotungwa bila kupatiwa elimu ya kutosha.
“Unaona fuso dogo kama lile,huwezi amini ni sh.500,000 kikweli ni kubwa ,sasa unakuta tunalalamika kutokana na kwamba hatujui lolote kuhusu sheria zao”
“Halafu hatujafundishwa kufunga hooks wanavyotaka wao wakala wa barabara,kila mtu anaufungaji wake lakini endapo watatuelewesha vizuri haina shida .
“Sasa wao wanapanda juu ya gari na kuchokonoa  chokono matokeo yake ndio inakuwa shida ,mchanga unamwagika”alisema Shao.
Magari aliutaka wakala huo kukagua kwa macho na sio kupekenyua maturubai kwa kuingiza mikono kwani kwa kufanya hivyo ni lazima mchanga mwagike .

No comments:

Post a Comment