KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 9, 2016

MASAUNI ALITAKA JESHI LA MAGEREZA KUTEKA SOKO NDANI YA NCHI

sau1
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni alipowasili katika Gereza Kuu la Karanga, Mkoani Kilimanjaro wakati alipotembelea  kiwanda cha viatu kilichopo gerezani haapo ili kujionea uzalishaji wa bidhaa mbalimbali hasa viatu. Naibu Waziri huyo amelitaka Jeshi hilo kuzidi kuboresha bidhaa za viatu hivyo ili kujipatia soko kubwa ndanni ya nchi na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini yanattumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.
sau2
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni  akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Karanga, Kamishna Msaaidizi Mkwiche  mkoani Kilimanjaro wakati alipofanya ziara katikaa Kiwanda cha viatu kilichopo katika gereza hilo ili kujionea  uzalishaji wa bidhaa za viatu ambavyo Rais Magufuli alitaka majeshi yote nchini kutumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.
sau3
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni akisikiliza maelezo kuhusu uzalishaji wa viatu katika kIwanda cha Gereza la Karanga kutoka kwa Fundi Mkuu wa Kiwanda hicho Ali Jambaraga wakati alipofanya ziara yake kwenda kujionea uzalishaji wa bidhaa mbalimbali lakini pia  ametaka  wazidi kuzalisha bidhaa bora zaidi ili kuteka soko la ndani na je ya nchi ikiwa ni pamoja na kutekeleza agizo la Rais Magufuli kuhakikisha majeshi yote nchini kutumia viatu vinavyotengenezwa na Jeshi la Magereza.

No comments:

Post a Comment